< Ufunuo 3 >

1 Kwa malaika wa kanisa la Sardi andika: 'Maneno ya yule anayeshikilia zile roho saba za Mungu na nyota saba. “Najua ambacho umefanya. Una sifa ya kuwa hai, lakini u-mfu.
“To the angel of the church in Sardis write: ‘These are the words of him who has the seven spirits of God and the seven stars: I know yoʋr works; yoʋ have a reputation for being alive, but yoʋ are dead.
2 Amka na kuimarisha yaliyosalia, lakini yako karibu kufa, kwa sababu sikuyaona matendo yako yamekamilika machoni pa Mungu wangu.
Be watchful and strengthen what remains, which yoʋ were about to throw away, for I have not found yoʋr works to be complete in the sight of my God.
3 Kwa hiyo, kumbuka, yale uliyoyapokea na kusikia. Yatii na kutubu. Lakini usipoamka, nitakuja kama mwivi, na hutajua saa ipi nitakayokuja juu yako.
So remember what yoʋ have received and heard; obey it and repent. If yoʋ do not wake up, I will come upon yoʋ like a thief, and yoʋ will certainly not know at what hour I will come upon yoʋ.
4 Lakini kuna majina machache ya watu katika Sardi ambao hawakuchafua nguo zao. Watatembea pamoja nami, wamevaa nguo nyeupe, kwa sababu wanastahili.
But yoʋ have a few individuals in Sardis who have not defiled their garments. They will walk with me in white, for they are worthy.
5 Yeye ashindaye atavikwa mavazi meupe, na kamwe sitalifuta jina lake kutoka katika kitabu cha uzima, na nitalitaja jina lake mbele ya Baba yangu, na mbele ya malaika.
He who overcomes will be clothed in white garments. I will certainly not blot out his name from the book of life, but will confess his name before my Father and before his angels.
6 Ukiwa na sikio, sikiliza Roho ayaambiavyo makanisa.”
He who has an ear, let him hear what the Spirit is saying to the churches.’
7 “Kwa malaika wa kanisa la Philadefia andika: Maneno ya aliye mtakatifu na kweli - aliye na funguo za Daudi, hufungua na hakuna afungaye, hufunga na hakuna awezaye kufungua.
“To the angel of the church in Philadelphia write: ‘These are the words of him who is holy and true, who has the key of David and opens doors that no one else can open or shut:
8 Najua ambacho umetenda. Tazama, nimekuwekea mbele yako mlango uliofunguliwa ambao hakuna awezaye kuufunga. Najua unazo nguvu kidogo, lakini umelitii neno langu na hujalikana jina langu.
I know yoʋr works. Behold, I have set before yoʋ an open door that no one can shut. I know that yoʋ have little strength, but yoʋ have kept my word and have not denied my name.
9 Angalia! Wote walio wa sinagogi la shetani, wale wasemao wao ni Wayahudi na kumbe siyo, badala yake wanadanganya. Nitawafanya waje na kusujudu mbele ya miguu yako, na watajua ya kuwa nilikupenda.
Those of the synagogue of Satan are liars. They declare themselves to be Jews but are not. Behold, I will make them come and bow down at yoʋr feet, and they will know that I love yoʋ.
10 Kwa kuwa umetunza amri yangu kwa uvumilivu wa uthabiti, nitakulinda pia katika saa yako ya kujaribiwa ambayo inakuja katika ulimwengu wote, kuwajaribu wale wote wanaoishi katika nchi.
Because yoʋ have kept my command to persevere, I will keep yoʋ from the hour of trial that is about to come upon the whole world to test those who dwell on the earth.
11 Naja upesi. Shikilia sana kile ulichonacho ili asiwepo mtu wa kuitwaa taji yako.
I am coming quickly. Hold fast to what yoʋ have so that no one will take yoʋr crown.
12 Nitamfanya yeye ashindaye kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, na hatatoka nje kamwe. Nitaliandika kwake jina la Mungu wangu, jina la mji wa Mungu wangu (Yerusalemu mpya, ushukao chini toka mbinguni kwa Mungu wangu), na jina langu jipya.
The one who overcomes I will make a pillar in the temple of my God, and he will no longer go out at all. I will write on him the name of my God, the name of the city of my God (the new Jerusalem that comes down out of heaven from my God), and my new name.
13 Yeye aliye na sikio, na asikie ambacho Roho anasema kwa makanisa.'
He who has an ear, let him hear what the Spirit is saying to the churches.’
14 “Kwa malaika wa kanisa la Laodikia andika: 'Maneno yake aliye Amina, wakutegemewa na shahidi mwaminifu, mtawala juu ya uumbaji wa Mungu.
“To the angel of the church in Laodicea write: ‘These are the words of the Amen, the faithful and true witness, the origin of God's creation:
15 Najua ambacho umefanya, na kwamba wewe si baridi wala moto, natamani kwamba ungekuwa wa baridi au moto!
I know yoʋr works; yoʋ are neither cold nor hot. If only yoʋ were cold or hot!
16 Hivyo, kwa sababu wewe ni vuguvugu, si moto wala baridi, nitakutapika utoke kinywani mwangu.
So, because yoʋ are lukewarm, and not hot or cold, I am about to spit yoʋ out of my mouth.
17 Kwa kuwa unasema, “Mimi ni tajiri, nimekuwa na mali nyingi, na sihitaji chochote.” Lakini hujui kwamba wewe ni duni sana, wakuhuzunikiwa, maskini, kipofu na uchi.
For yoʋ say, “I am rich; I have become wealthy and need nothing,” but yoʋ do not realize that yoʋ are wretched, pitiful, poor, blind, and naked.
18 Sikiliza ushauri kwangu: Nunua kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto ili upate kuwa tajiri, na nguo nyeupe za kumetameta ili ujivike mwenyewe na usioneshe aibu ya uchi wako, na mafuta ya kupaka katika macho yako upate kuona.
I counsel yoʋ to buy from me gold refined by fire so that yoʋ may be rich, and white garments so that yoʋ may clothe yoʋrself and the shame of yoʋr nakedness may not be revealed, and eye salve to anoint yoʋr eyes so that yoʋ may see.
19 Kila nimpendaye, namwelekeza na kuwafundisha namna iwapasavyo kuishi; kwa hiyo, kuwa mkweli na kutubu.
Those whom I love, I reprove and discipline. Therefore be zealous and repent.
20 Tazama nasimama katika mlango na kubisha. Yeyote asikiaye sauti yangu na kufungua mlango, nitakuja na kuingia nyumbani kwake, na kula chakula naye na yeye pamoja nami.
Behold, I stand at the door and knock. If anyone hears my voice and opens the door, I will come in to him and dine with him, and he with me.
21 Yeye ashindaye, nitampa haki ya kukaa chini pamoja nami juu ya kiti changu cha enzi, kama vile mimi nilivyoshinda na kukaa chini pamoja na Baba yangu juu ya kiti chake cha enzi.
To him who overcomes I will give the right to sit with me on my throne, just as I overcame and sat down with my Father on his throne.
22 Yeye aliye na sikio, na asikilize ambacho Roho ayaambia makanisa.”
He who has an ear, let him hear what the Spirit is saying to the churches.’”

< Ufunuo 3 >