< Ufunuo 3 >

1 Kwa malaika wa kanisa la Sardi andika: 'Maneno ya yule anayeshikilia zile roho saba za Mungu na nyota saba. “Najua ambacho umefanya. Una sifa ya kuwa hai, lakini u-mfu.
AND to the angel who is in Sardis write: These saith he who hath the seven Spirits of Aloha, and the seven stars: I know thy works, that a name thou hast that thou livest, and thou art dead.
2 Amka na kuimarisha yaliyosalia, lakini yako karibu kufa, kwa sababu sikuyaona matendo yako yamekamilika machoni pa Mungu wangu.
Awake, and keep those things which remain, which are about to die; for I have not found thy works complete before my God.
3 Kwa hiyo, kumbuka, yale uliyoyapokea na kusikia. Yatii na kutubu. Lakini usipoamka, nitakuja kama mwivi, na hutajua saa ipi nitakayokuja juu yako.
Remember then how thou hast received, and hearken, and keep, and repent. And if then thou wilt not awake, I will come against thee as the thief, and thou shalt not know in what hour I come against thee.
4 Lakini kuna majina machache ya watu katika Sardi ambao hawakuchafua nguo zao. Watatembea pamoja nami, wamevaa nguo nyeupe, kwa sababu wanastahili.
But thou hast a few names in Sardis who have not defiled their vestments; and they shall walk with me in white, because they are worthy.
5 Yeye ashindaye atavikwa mavazi meupe, na kamwe sitalifuta jina lake kutoka katika kitabu cha uzima, na nitalitaja jina lake mbele ya Baba yangu, na mbele ya malaika.
He who overcometh shall be clothed in white vestments, and I will not blot their name from the book of life; and I will confess their name before my Father, and before his angels.
6 Ukiwa na sikio, sikiliza Roho ayaambiavyo makanisa.”
He who hath ears, let him hear what the Spirit saith to the churches.
7 “Kwa malaika wa kanisa la Philadefia andika: Maneno ya aliye mtakatifu na kweli - aliye na funguo za Daudi, hufungua na hakuna afungaye, hufunga na hakuna awezaye kufungua.
And to the angel of the church which is in Philadelphia write: These saith the Holy, the True, who hath the key of David; who openeth and no man shutteth, and who shutteth and no man openeth.
8 Najua ambacho umetenda. Tazama, nimekuwekea mbele yako mlango uliofunguliwa ambao hakuna awezaye kuufunga. Najua unazo nguvu kidogo, lakini umelitii neno langu na hujalikana jina langu.
I know thy works; and, behold, I have given before thee an open door, which no man can shut; because thou hast a little strength, and hast kept my word, and hast not denied my name.
9 Angalia! Wote walio wa sinagogi la shetani, wale wasemao wao ni Wayahudi na kumbe siyo, badala yake wanadanganya. Nitawafanya waje na kusujudu mbele ya miguu yako, na watajua ya kuwa nilikupenda.
Behold, I will give of the synagogue of Satana, who say that they are Jihudoyee, and are not, but lie; behold, I will make them to come and worship before thy feet, and they shall know that I have loved thee.
10 Kwa kuwa umetunza amri yangu kwa uvumilivu wa uthabiti, nitakulinda pia katika saa yako ya kujaribiwa ambayo inakuja katika ulimwengu wote, kuwajaribu wale wote wanaoishi katika nchi.
Because thou hast kept the word of my patience, I will keep thee from the hour of temptation, which is to come upon all the habitable world, to try them who dwell upon the earth.
11 Naja upesi. Shikilia sana kile ulichonacho ili asiwepo mtu wa kuitwaa taji yako.
I come quickly. Hold that which thou hast, that no man take thy crown.
12 Nitamfanya yeye ashindaye kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, na hatatoka nje kamwe. Nitaliandika kwake jina la Mungu wangu, jina la mji wa Mungu wangu (Yerusalemu mpya, ushukao chini toka mbinguni kwa Mungu wangu), na jina langu jipya.
Him who overcometh I will make a column in the temple of my God, and he shall go out no more; and I will write upon him the name of my God, and of Urishlem the new, which descendeth from heaven from my God, and my new name.
13 Yeye aliye na sikio, na asikie ambacho Roho anasema kwa makanisa.'
He who hath ears, let him hear what the Spirit saith to the churches.
14 “Kwa malaika wa kanisa la Laodikia andika: 'Maneno yake aliye Amina, wakutegemewa na shahidi mwaminifu, mtawala juu ya uumbaji wa Mungu.
And to the angel of the church which is in Ladikia write: These saith the Amen, the Witness, the faithful, the true, the Head of the creation of Aloha.
15 Najua ambacho umefanya, na kwamba wewe si baridi wala moto, natamani kwamba ungekuwa wa baridi au moto!
I know thy works, that thou art neither hot nor cold. Would that thou wast cold or hot!
16 Hivyo, kwa sababu wewe ni vuguvugu, si moto wala baridi, nitakutapika utoke kinywani mwangu.
So, because thou art lukewarm, and neither hot nor cold, I will vomit thee from my mouth.
17 Kwa kuwa unasema, “Mimi ni tajiri, nimekuwa na mali nyingi, na sihitaji chochote.” Lakini hujui kwamba wewe ni duni sana, wakuhuzunikiwa, maskini, kipofu na uchi.
Because thou sayest, I am rich, and have become opulent, and of nothing have need; and knowest not that thou art infirm, and miserable, and needy, and blind, and naked;
18 Sikiliza ushauri kwangu: Nunua kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto ili upate kuwa tajiri, na nguo nyeupe za kumetameta ili ujivike mwenyewe na usioneshe aibu ya uchi wako, na mafuta ya kupaka katika macho yako upate kuona.
I counsel thee to buy of me gold, proved by fire, that thou mayest be rich; and white raiment, that thou mayest be clothed, and the shame of thy nakedness be not seen; and lave with collyrium thine eyes, that thou mayest see.
19 Kila nimpendaye, namwelekeza na kuwafundisha namna iwapasavyo kuishi; kwa hiyo, kuwa mkweli na kutubu.
All those whom I love, I reprove and chasten: be zealous therefore, and repent.
20 Tazama nasimama katika mlango na kubisha. Yeyote asikiaye sauti yangu na kufungua mlango, nitakuja na kuingia nyumbani kwake, na kula chakula naye na yeye pamoja nami.
Behold, I stand at the door and knock: if any man hear my voice, and will open the door, I will enter unto him, and will sup with him, and he with me.
21 Yeye ashindaye, nitampa haki ya kukaa chini pamoja nami juu ya kiti changu cha enzi, kama vile mimi nilivyoshinda na kukaa chini pamoja na Baba yangu juu ya kiti chake cha enzi.
And to him who overcometh I will give to sit with me upon my throne, as also I have overcome, and have sat with my Father in his throne.
22 Yeye aliye na sikio, na asikilize ambacho Roho ayaambia makanisa.”
He who hath ears, let him hear what the Spirit saith to the churches.

< Ufunuo 3 >