< Ufunuo 3 >

1 Kwa malaika wa kanisa la Sardi andika: 'Maneno ya yule anayeshikilia zile roho saba za Mungu na nyota saba. “Najua ambacho umefanya. Una sifa ya kuwa hai, lakini u-mfu.
And to the angel of the in Sardis church do write: These things says the [One] having the seven Spirits of God and the seven stars; I know your deeds that characterization you have that you are alive and yet dead you are.
2 Amka na kuimarisha yaliyosalia, lakini yako karibu kufa, kwa sababu sikuyaona matendo yako yamekamilika machoni pa Mungu wangu.
do be watching and do strengthen the [things] that remain which (were about *N+k+O) (to die; *NK+O) not for I have found your works completed in the sight of the God (of Mine. *NO)
3 Kwa hiyo, kumbuka, yale uliyoyapokea na kusikia. Yatii na kutubu. Lakini usipoamka, nitakuja kama mwivi, na hutajua saa ipi nitakayokuja juu yako.
do remember therefore what you have received and heard — and do keep [it] and do repent. If therefore not you shall watch, I will come (upon you *K) like a thief, and certainly not (you may know *NK+o) at what hour I will come upon you.
4 Lakini kuna majina machache ya watu katika Sardi ambao hawakuchafua nguo zao. Watatembea pamoja nami, wamevaa nguo nyeupe, kwa sababu wanastahili.
(But *NO) you have a few people in Sardis who not soiled the garments of them, and they will walk with Me in white, because worthy they are.
5 Yeye ashindaye atavikwa mavazi meupe, na kamwe sitalifuta jina lake kutoka katika kitabu cha uzima, na nitalitaja jina lake mbele ya Baba yangu, na mbele ya malaika.
The [one] overcoming (thus *N+kO) will be clothed in garments white, And certainly not will I blot out the name of him from the book of life and (I will acknowledge *N+kO) the name of him before the Father of Mine and before the angels of Him.
6 Ukiwa na sikio, sikiliza Roho ayaambiavyo makanisa.”
The [one] having an ear he should hear what the Spirit says to the churches.
7 “Kwa malaika wa kanisa la Philadefia andika: Maneno ya aliye mtakatifu na kweli - aliye na funguo za Daudi, hufungua na hakuna afungaye, hufunga na hakuna awezaye kufungua.
And to the angel of the in Philadelphia church do write: These things says the Holy [One], the True [One], who is having the key of David, who is opening and no [one] (will shut *N+kO) (it (only except that which is being open); *O) and (shutting *N+kO) and no [one] (opens; *NK+o)
8 Najua ambacho umetenda. Tazama, nimekuwekea mbele yako mlango uliofunguliwa ambao hakuna awezaye kuufunga. Najua unazo nguvu kidogo, lakini umelitii neno langu na hujalikana jina langu.
I know your deeds. Behold I have set before you a door opened (which *N+KO) no [one] is able to shut it; because little you have power and yet you have kept My word and not denied the name of Me.
9 Angalia! Wote walio wa sinagogi la shetani, wale wasemao wao ni Wayahudi na kumbe siyo, badala yake wanadanganya. Nitawafanya waje na kusujudu mbele ya miguu yako, na watajua ya kuwa nilikupenda.
Behold (I may give *N+kO) [those] from the synagogue of Satan — those declaring themselves Jews to be and not are, but they lie — behold I will cause them that (they will come *N+kO) and (they will worship *N+kO) before the feet of you and they may know that I myself loved you.
10 Kwa kuwa umetunza amri yangu kwa uvumilivu wa uthabiti, nitakulinda pia katika saa yako ya kujaribiwa ambayo inakuja katika ulimwengu wote, kuwajaribu wale wote wanaoishi katika nchi.
Because you have kept the word of the patient endurance of Mine, I myself also I myself also you will keep out of the hour of the trial which is being about to come upon the inhabited world whole to try those dwelling upon the earth.
11 Naja upesi. Shikilia sana kile ulichonacho ili asiwepo mtu wa kuitwaa taji yako.
(behold *K) I am coming quickly; do hold fast to what you have, so that no one may take the crown of you.
12 Nitamfanya yeye ashindaye kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, na hatatoka nje kamwe. Nitaliandika kwake jina la Mungu wangu, jina la mji wa Mungu wangu (Yerusalemu mpya, ushukao chini toka mbinguni kwa Mungu wangu), na jina langu jipya.
The [one] overcoming, I will make him a pillar in the temple of the God of Mine, and out certainly not shall he go anymore, And I will write upon him the name of the God of Mine and the name of the city of the God of Mine, the new Jerusalem, which (is descending *NK+o) out of heaven from the God of Mine, and the name of Me new.
13 Yeye aliye na sikio, na asikie ambacho Roho anasema kwa makanisa.'
The [one] having an ear he should hear what the Spirit says to the churches.
14 “Kwa malaika wa kanisa la Laodikia andika: 'Maneno yake aliye Amina, wakutegemewa na shahidi mwaminifu, mtawala juu ya uumbaji wa Mungu.
And to the angel of the (in *no) (Laodicea *N+KO) church do write: These things says the Amen, the Witness faithful and true, the Beginning of the creation of God;
15 Najua ambacho umefanya, na kwamba wewe si baridi wala moto, natamani kwamba ungekuwa wa baridi au moto!
I know your works that neither cold you are nor hot. I wish cold (you were *N+kO) or hot;
16 Hivyo, kwa sababu wewe ni vuguvugu, si moto wala baridi, nitakutapika utoke kinywani mwangu.
So because lukewarm you are and (neither *NK+o) hot nor cold, I am about you to spit out of the mouth of Mine,
17 Kwa kuwa unasema, “Mimi ni tajiri, nimekuwa na mali nyingi, na sihitaji chochote.” Lakini hujui kwamba wewe ni duni sana, wakuhuzunikiwa, maskini, kipofu na uchi.
For you say that Rich I am and I have grown rich and ([of] no [thing] *N+kO) need I have, And not do you understand that you yourself are wretched and miserable and poor and blind and naked,
18 Sikiliza ushauri kwangu: Nunua kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto ili upate kuwa tajiri, na nguo nyeupe za kumetameta ili ujivike mwenyewe na usioneshe aibu ya uchi wako, na mafuta ya kupaka katika macho yako upate kuona.
I counsel you to buy from Me gold refined by fire so that you may be rich, and garments white so that you may be clothed and not may be made manifest the shame of the nakedness of you, and eye-salve (so that *o) (to anoint *N+k+O) the eyes of you so that you may see.
19 Kila nimpendaye, namwelekeza na kuwafundisha namna iwapasavyo kuishi; kwa hiyo, kuwa mkweli na kutubu.
I myself as many as if shall love I rebuke and discipline. (do be jealous *N+kO) therefore and do repent.
20 Tazama nasimama katika mlango na kubisha. Yeyote asikiaye sauti yangu na kufungua mlango, nitakuja na kuingia nyumbani kwake, na kula chakula naye na yeye pamoja nami.
Behold I have stood at the door and knock. If anyone shall hear the voice of Mine and shall open the door, (then *no) I will come in to him and I will dine with him and he with Me.
21 Yeye ashindaye, nitampa haki ya kukaa chini pamoja nami juu ya kiti changu cha enzi, kama vile mimi nilivyoshinda na kukaa chini pamoja na Baba yangu juu ya kiti chake cha enzi.
The [one] overcoming, I will give to him to sit with Me on the throne of Mine as I myself also I myself also overcame and I sat down with the Father of Mine on the throne of Him.
22 Yeye aliye na sikio, na asikilize ambacho Roho ayaambia makanisa.”
The [one] having an ear he should hear what the Spirit says to the churches.

< Ufunuo 3 >