< Ufunuo 3 >

1 Kwa malaika wa kanisa la Sardi andika: 'Maneno ya yule anayeshikilia zile roho saba za Mungu na nyota saba. “Najua ambacho umefanya. Una sifa ya kuwa hai, lakini u-mfu.
‘To the angel of the church in Sardis write: These are the words of him who has the seven spirits of God and the seven stars; – I know your life, and that people say of you that you are living, though you are dead.
2 Amka na kuimarisha yaliyosalia, lakini yako karibu kufa, kwa sababu sikuyaona matendo yako yamekamilika machoni pa Mungu wangu.
Be on the watch, and strengthen what still survives, though once it was all but dead; for I have not found your life perfect in the eyes of my God.
3 Kwa hiyo, kumbuka, yale uliyoyapokea na kusikia. Yatii na kutubu. Lakini usipoamka, nitakuja kama mwivi, na hutajua saa ipi nitakayokuja juu yako.
Therefore remember what you have received and heard, and lay it to heart and repent. Unless you are on the watch, I will come like a thief, and you will not know at what hour I am coming to you.
4 Lakini kuna majina machache ya watu katika Sardi ambao hawakuchafua nguo zao. Watatembea pamoja nami, wamevaa nguo nyeupe, kwa sababu wanastahili.
Yet there are some few among you at Sardis who did not soil their robes; they will walk with me, robed in white, for they are worthy.
5 Yeye ashindaye atavikwa mavazi meupe, na kamwe sitalifuta jina lake kutoka katika kitabu cha uzima, na nitalitaja jina lake mbele ya Baba yangu, na mbele ya malaika.
Those who conquer will be clothed in these white robes, and I will not strike their name out of the book of life; but I will own them before my Father, and before his angels.
6 Ukiwa na sikio, sikiliza Roho ayaambiavyo makanisa.”
Let those who have ears hear what the Spirit is saying to the churches.
7 “Kwa malaika wa kanisa la Philadefia andika: Maneno ya aliye mtakatifu na kweli - aliye na funguo za Daudi, hufungua na hakuna afungaye, hufunga na hakuna awezaye kufungua.
‘To the angel of the church in Philadelphia write: These are the words of him who is holy and true, who holds the Key of David, who opens and no one will shut, and shuts and no one opens:
8 Najua ambacho umetenda. Tazama, nimekuwekea mbele yako mlango uliofunguliwa ambao hakuna awezaye kuufunga. Najua unazo nguvu kidogo, lakini umelitii neno langu na hujalikana jina langu.
I know your life (see, I have set a door open before you which no one is able to shut), I know that, though you have but little strength, you kept my teaching in mind, and did not disown my name.
9 Angalia! Wote walio wa sinagogi la shetani, wale wasemao wao ni Wayahudi na kumbe siyo, badala yake wanadanganya. Nitawafanya waje na kusujudu mbele ya miguu yako, na watajua ya kuwa nilikupenda.
Listen, I give some of the congregation of Satan, the people who declare that they are God’s people, though they are not, but are lying – I will make them come and bow down at your feet, and they will learn that I loved you.
10 Kwa kuwa umetunza amri yangu kwa uvumilivu wa uthabiti, nitakulinda pia katika saa yako ya kujaribiwa ambayo inakuja katika ulimwengu wote, kuwajaribu wale wote wanaoishi katika nchi.
Because you kept in mind the story of my endurance, I will keep you in the hour of trial that is about to come on the whole world, the hour that will test all who are living on earth.
11 Naja upesi. Shikilia sana kile ulichonacho ili asiwepo mtu wa kuitwaa taji yako.
I will come quickly. Hold to what you have received so that no one may take your crown.
12 Nitamfanya yeye ashindaye kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, na hatatoka nje kamwe. Nitaliandika kwake jina la Mungu wangu, jina la mji wa Mungu wangu (Yerusalemu mpya, ushukao chini toka mbinguni kwa Mungu wangu), na jina langu jipya.
Those who conquer – I will make them a pillar in the Temple of my God; and never more will they leave it; and I will write on them the name of my God and the name of the city of my God, the New Jerusalem, which is coming down out of heaven from my God, and I will write on them my new name.
13 Yeye aliye na sikio, na asikie ambacho Roho anasema kwa makanisa.'
Let those who have ears hear what the Spirit is saying to the churches.
14 “Kwa malaika wa kanisa la Laodikia andika: 'Maneno yake aliye Amina, wakutegemewa na shahidi mwaminifu, mtawala juu ya uumbaji wa Mungu.
‘To the angel of the church in Laodicea write: These are the words of the Unchanging One, the witness faithful and true, the beginning of the Creation of God:
15 Najua ambacho umefanya, na kwamba wewe si baridi wala moto, natamani kwamba ungekuwa wa baridi au moto!
I know your life; I know that you are neither cold nor hot. If only you were either cold or hot!
16 Hivyo, kwa sababu wewe ni vuguvugu, si moto wala baridi, nitakutapika utoke kinywani mwangu.
But now, because you are lukewarm, neither hot nor cold, I am about to spit you out of my mouth.
17 Kwa kuwa unasema, “Mimi ni tajiri, nimekuwa na mali nyingi, na sihitaji chochote.” Lakini hujui kwamba wewe ni duni sana, wakuhuzunikiwa, maskini, kipofu na uchi.
You say “I am rich and have grown rich, and I want for nothing,” and you do not know that you are wretched, miserable, poor, blind, naked!
18 Sikiliza ushauri kwangu: Nunua kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto ili upate kuwa tajiri, na nguo nyeupe za kumetameta ili ujivike mwenyewe na usioneshe aibu ya uchi wako, na mafuta ya kupaka katika macho yako upate kuona.
Therefore I counsel you to buy from me gold which has been refined by fire so that you may grow rich; and white robes, so that you may be clothed and your shameful nakedness be hidden; and ointment to anoint your eyes, so that you may see.
19 Kila nimpendaye, namwelekeza na kuwafundisha namna iwapasavyo kuishi; kwa hiyo, kuwa mkweli na kutubu.
All whom I love I rebuke and discipline. Therefore be in earnest and repent.
20 Tazama nasimama katika mlango na kubisha. Yeyote asikiaye sauti yangu na kufungua mlango, nitakuja na kuingia nyumbani kwake, na kula chakula naye na yeye pamoja nami.
I am standing at the door and knocking! If anyone hears my voice and opens the door, I will go in, and will feast with them, and they will feast with me.
21 Yeye ashindaye, nitampa haki ya kukaa chini pamoja nami juu ya kiti changu cha enzi, kama vile mimi nilivyoshinda na kukaa chini pamoja na Baba yangu juu ya kiti chake cha enzi.
To those who conquer – to them I will give the right to sit beside me on my throne, as I, when I conquered, took my seat beside my Father on his throne.
22 Yeye aliye na sikio, na asikilize ambacho Roho ayaambia makanisa.”
Let those who have ears hear what the Spirit is saying to the churches.’

< Ufunuo 3 >