< Ufunuo 3 >

1 Kwa malaika wa kanisa la Sardi andika: 'Maneno ya yule anayeshikilia zile roho saba za Mungu na nyota saba. “Najua ambacho umefanya. Una sifa ya kuwa hai, lakini u-mfu.
And to the angel of the church in Sardis write; The one having the seven Spirits of God, and the seven stars, says these things; I know your works, that you have a name that you are living, and are dead.
2 Amka na kuimarisha yaliyosalia, lakini yako karibu kufa, kwa sababu sikuyaona matendo yako yamekamilika machoni pa Mungu wangu.
Be you watchful, and strengthen the remaining things, which are about to die. For I have not found your works perfect before my God.
3 Kwa hiyo, kumbuka, yale uliyoyapokea na kusikia. Yatii na kutubu. Lakini usipoamka, nitakuja kama mwivi, na hutajua saa ipi nitakayokuja juu yako.
Remember therefore how you have received and heard, and hold fast, and repent. If you do not watch, I will come as a thief, and you shall not know what hour I will come upon you.
4 Lakini kuna majina machache ya watu katika Sardi ambao hawakuchafua nguo zao. Watatembea pamoja nami, wamevaa nguo nyeupe, kwa sababu wanastahili.
But you have a few names in Sardis who have not defiled their garments; and they shall walk with me in white: because they are worthy.
5 Yeye ashindaye atavikwa mavazi meupe, na kamwe sitalifuta jina lake kutoka katika kitabu cha uzima, na nitalitaja jina lake mbele ya Baba yangu, na mbele ya malaika.
The one conquering shall thus be clothed in white garments; and I will not blot out his name from the book of life, and I will confess his name before my Father, and in the presence of his angels.
6 Ukiwa na sikio, sikiliza Roho ayaambiavyo makanisa.”
Let the one having ears hear what the Spirit says to the churches.
7 “Kwa malaika wa kanisa la Philadefia andika: Maneno ya aliye mtakatifu na kweli - aliye na funguo za Daudi, hufungua na hakuna afungaye, hufunga na hakuna awezaye kufungua.
And to the angel of the church in Philadelphia write; The holy, true one, the one having the key of David, the one opening, and no one shall shut; and the one shutting, and no one shall open; says these things.
8 Najua ambacho umetenda. Tazama, nimekuwekea mbele yako mlango uliofunguliwa ambao hakuna awezaye kuufunga. Najua unazo nguvu kidogo, lakini umelitii neno langu na hujalikana jina langu.
I know your works; behold, I have given before you an open door, which no one is able to shut: and you have a little power, and you have kept my word, and not denied my name.
9 Angalia! Wote walio wa sinagogi la shetani, wale wasemao wao ni Wayahudi na kumbe siyo, badala yake wanadanganya. Nitawafanya waje na kusujudu mbele ya miguu yako, na watajua ya kuwa nilikupenda.
Behold, I give of the synagogue of Satan, those who say they are Jews, and are not, but are lying; behold, I will make them that they shall come and worship before thy feet, and may know that I have loved thee with divine love.
10 Kwa kuwa umetunza amri yangu kwa uvumilivu wa uthabiti, nitakulinda pia katika saa yako ya kujaribiwa ambayo inakuja katika ulimwengu wote, kuwajaribu wale wote wanaoishi katika nchi.
Because you have kept the word of my patience, and I will keep you from the hour of temptation, which is about to come upon the whole world, to try those dwelling upon the earth.
11 Naja upesi. Shikilia sana kile ulichonacho ili asiwepo mtu wa kuitwaa taji yako.
I am coming quickly: hold fast that which you have, that no one may take your crown.
12 Nitamfanya yeye ashindaye kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, na hatatoka nje kamwe. Nitaliandika kwake jina la Mungu wangu, jina la mji wa Mungu wangu (Yerusalemu mpya, ushukao chini toka mbinguni kwa Mungu wangu), na jina langu jipya.
The one conquering, I will make him a pillar in the temple of my God, and he shall go out no more: and I will write upon him the name of my God, and the name of the city of my God, the new Jerusalem, which is coming down out of heaven from my God: and my new name.
13 Yeye aliye na sikio, na asikie ambacho Roho anasema kwa makanisa.'
Let the one having ears, hear what the Spirit says to the churches.
14 “Kwa malaika wa kanisa la Laodikia andika: 'Maneno yake aliye Amina, wakutegemewa na shahidi mwaminifu, mtawala juu ya uumbaji wa Mungu.
And to the angel of the church in Laodicea write; The Amen, the faithful and true witness, the beginning of the creation of God, says these things;
15 Najua ambacho umefanya, na kwamba wewe si baridi wala moto, natamani kwamba ungekuwa wa baridi au moto!
I know your works, that you are neither cold nor hot. I would that you were either cold or hot.
16 Hivyo, kwa sababu wewe ni vuguvugu, si moto wala baridi, nitakutapika utoke kinywani mwangu.
Thus because you are lukewarm, and neither hot nor cold, I am about to spew you out of my mouth.
17 Kwa kuwa unasema, “Mimi ni tajiri, nimekuwa na mali nyingi, na sihitaji chochote.” Lakini hujui kwamba wewe ni duni sana, wakuhuzunikiwa, maskini, kipofu na uchi.
Because you are saying, That I am rich, and have increased in riches, and have need as to nothing, and do you not know that you are miserable, and pitiful, and poor, and blind, and naked?
18 Sikiliza ushauri kwangu: Nunua kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto ili upate kuwa tajiri, na nguo nyeupe za kumetameta ili ujivike mwenyewe na usioneshe aibu ya uchi wako, na mafuta ya kupaka katika macho yako upate kuona.
I counsel you to buy from me gold which has been purified by the fire, in order that you may be rich; and white garments, in order that you may be clothed, and the shame of your nakedness may not be exposed; and eye salve to anoint your eyes, that you may see.
19 Kila nimpendaye, namwelekeza na kuwafundisha namna iwapasavyo kuishi; kwa hiyo, kuwa mkweli na kutubu.
So many as I love, I rebuke and chastise; be zealous, and repent.
20 Tazama nasimama katika mlango na kubisha. Yeyote asikiaye sauti yangu na kufungua mlango, nitakuja na kuingia nyumbani kwake, na kula chakula naye na yeye pamoja nami.
Behold, I stand at the door, and am knocking: if any one may hear my voice, and may open the door, I will come in unto him, and will sup with him, and he with me.
21 Yeye ashindaye, nitampa haki ya kukaa chini pamoja nami juu ya kiti changu cha enzi, kama vile mimi nilivyoshinda na kukaa chini pamoja na Baba yangu juu ya kiti chake cha enzi.
The one conquering, I will give unto him to sit with me on my throne, as I indeed have conquered, and sat down with my Father on his throne.
22 Yeye aliye na sikio, na asikilize ambacho Roho ayaambia makanisa.”
Let the one having ears hear what the Spirit says to the churches.

< Ufunuo 3 >