< Ufunuo 3 >

1 Kwa malaika wa kanisa la Sardi andika: 'Maneno ya yule anayeshikilia zile roho saba za Mungu na nyota saba. “Najua ambacho umefanya. Una sifa ya kuwa hai, lakini u-mfu.
And to the agent of the congregation in Sardis write, These things says he who has the seven Spirits of God, and the seven stars: I know thy works, that thou have a name that thou live, and thou are dead.
2 Amka na kuimarisha yaliyosalia, lakini yako karibu kufa, kwa sababu sikuyaona matendo yako yamekamilika machoni pa Mungu wangu.
Become thou watchful, and strengthen the remaining things that thou were going to throw away, for I have not found thy works made complete before my God.
3 Kwa hiyo, kumbuka, yale uliyoyapokea na kusikia. Yatii na kutubu. Lakini usipoamka, nitakuja kama mwivi, na hutajua saa ipi nitakayokuja juu yako.
Remember therefore how thou have received and heard, and be on guard, and repent. If therefore thou will not watch, I will come upon thee as a thief, and thou will, no, not know what hour I will come upon thee.
4 Lakini kuna majina machache ya watu katika Sardi ambao hawakuchafua nguo zao. Watatembea pamoja nami, wamevaa nguo nyeupe, kwa sababu wanastahili.
But thou have a few names in Sardis who did not defile their garments. And they will walk with me in white, because they are worthy.
5 Yeye ashindaye atavikwa mavazi meupe, na kamwe sitalifuta jina lake kutoka katika kitabu cha uzima, na nitalitaja jina lake mbele ya Baba yangu, na mbele ya malaika.
He who overcomes, this man will be clothed in white garments, and I will, no, not erase his name out of the book of life. And I will acknowledge his name before my Father, and before his agents.
6 Ukiwa na sikio, sikiliza Roho ayaambiavyo makanisa.”
He who has an ear, let him hear what the Spirit says to the congregations.
7 “Kwa malaika wa kanisa la Philadefia andika: Maneno ya aliye mtakatifu na kweli - aliye na funguo za Daudi, hufungua na hakuna afungaye, hufunga na hakuna awezaye kufungua.
And to the agent of the congregation in Philadelphia write, These things says the Holy, the True, he who has the key of David, who opens, and none will shut it except he who opens, and none will open:
8 Najua ambacho umetenda. Tazama, nimekuwekea mbele yako mlango uliofunguliwa ambao hakuna awezaye kuufunga. Najua unazo nguvu kidogo, lakini umelitii neno langu na hujalikana jina langu.
I know thy works. Behold, I have given before thee an opened door that none is able to shut it, because thou have little power, and thou keep my word, and did not deny my name.
9 Angalia! Wote walio wa sinagogi la shetani, wale wasemao wao ni Wayahudi na kumbe siyo, badala yake wanadanganya. Nitawafanya waje na kusujudu mbele ya miguu yako, na watajua ya kuwa nilikupenda.
Behold, I give of the synagogue of Satan, those who say themselves to be Jews, and are not, but lie, behold, I will make them so that they will come and bow down before thy feet, and may know that I have loved thee.
10 Kwa kuwa umetunza amri yangu kwa uvumilivu wa uthabiti, nitakulinda pia katika saa yako ya kujaribiwa ambayo inakuja katika ulimwengu wote, kuwajaribu wale wote wanaoishi katika nchi.
Because thou keep the word of my perseverance, I also will keep thee from the hour of trial that is going to come upon the whole inhabited world, to try those who dwell upon the earth.
11 Naja upesi. Shikilia sana kile ulichonacho ili asiwepo mtu wa kuitwaa taji yako.
I come quickly, hold firm what thou have, so that none may take thy crown.
12 Nitamfanya yeye ashindaye kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, na hatatoka nje kamwe. Nitaliandika kwake jina la Mungu wangu, jina la mji wa Mungu wangu (Yerusalemu mpya, ushukao chini toka mbinguni kwa Mungu wangu), na jina langu jipya.
He who overcomes, I will make him a pillar in the temple of my God, and he will, no, not go out any more. And I will write upon him the name of my God, and the name of the city of my God, the new Jerusalem (it comes down out of the heaven from my God), and my new name.
13 Yeye aliye na sikio, na asikie ambacho Roho anasema kwa makanisa.'
He who has an ear, let him hear what the Spirit says to the congregations.
14 “Kwa malaika wa kanisa la Laodikia andika: 'Maneno yake aliye Amina, wakutegemewa na shahidi mwaminifu, mtawala juu ya uumbaji wa Mungu.
And to the agent of the congregation in Laodicea write, These things says the Truly, the faithful and true witness, the primacy of the creation of God:
15 Najua ambacho umefanya, na kwamba wewe si baridi wala moto, natamani kwamba ungekuwa wa baridi au moto!
I know thy works, that thou are neither cold nor hot. O that thou were cold or hot.
16 Hivyo, kwa sababu wewe ni vuguvugu, si moto wala baridi, nitakutapika utoke kinywani mwangu.
So because thou are lukewarm, and neither hot nor cold, I am going to spew thee out of my mouth.
17 Kwa kuwa unasema, “Mimi ni tajiri, nimekuwa na mali nyingi, na sihitaji chochote.” Lakini hujui kwamba wewe ni duni sana, wakuhuzunikiwa, maskini, kipofu na uchi.
Because thou say, I am rich, and have become wealthy, and have need of nothing, and do not know that thou are wretched and miserable and poor and blind and naked.
18 Sikiliza ushauri kwangu: Nunua kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto ili upate kuwa tajiri, na nguo nyeupe za kumetameta ili ujivike mwenyewe na usioneshe aibu ya uchi wako, na mafuta ya kupaka katika macho yako upate kuona.
I counsel thee to buy from me gold refined from fire, so that thou may become wealthy, and white garments, so that thou may clothe thyself, and the shame of thy nakedness may not be made known, and eye-salve, so that thou may anoint thine eyes, so that thou may see.
19 Kila nimpendaye, namwelekeza na kuwafundisha namna iwapasavyo kuishi; kwa hiyo, kuwa mkweli na kutubu.
As many as I love, I rebuke and chasten. Be zealous therefore, and repent.
20 Tazama nasimama katika mlango na kubisha. Yeyote asikiaye sauti yangu na kufungua mlango, nitakuja na kuingia nyumbani kwake, na kula chakula naye na yeye pamoja nami.
Behold, I stand at the door and knock. If any man hears my voice and opens the door, I will come in to him, and will dine with him, and he with me.
21 Yeye ashindaye, nitampa haki ya kukaa chini pamoja nami juu ya kiti changu cha enzi, kama vile mimi nilivyoshinda na kukaa chini pamoja na Baba yangu juu ya kiti chake cha enzi.
He who overcomes, I will give him to sit with me in my throne, as I also overcame, and sat down with my Father in his throne.
22 Yeye aliye na sikio, na asikilize ambacho Roho ayaambia makanisa.”
He who has an ear, let him hear what the Spirit says to the congregations.

< Ufunuo 3 >