< Zaburi 92 >

1 Ni jambo jema kumshukuru Yahwe na kuliimbia sifa jina lako, Uliye Juu,
Bueno es alabar a Yavé Y cantar salmos a tu Nombre, oh ʼElyón.
2 kutangaza uaminifu wa agano lako wakati wa asubuhi na uaminifu wako kila usiku,
Anunciar por la mañana tu misericordia Y tu fidelidad cada noche
3 kwa kinubi cha nyuzi kumi na kwa tuni ya kinubi.
Con el decacordio y el salterio, Con el armonioso tono del arpa.
4 Kwa kuwa wewe, Yahwe, matendo yako yamenifurahisha. Nitaimba kwa furaha kwa sababu ya matendo ya mikono yako.
Porque Tú, oh Yavé, me alegraste con lo que hiciste. Por las obras de tus manos doy gritos de júbilo.
5 Ni jinsi gani matendo yako ni makuu, Yahwe! mawazo yako ni ya kina.
¡Cuán grandes son tus obras, oh Yavé! Tus pensamientos son muy profundos.
6 Mtu mpumbavu hawezi kuyajua, wala mjinga kuyaelewa haya:
El hombre necio no sabe Y el insensato no entiende esto:
7 Wasio haki watakapochipuka kama nyasi, na hata watendao uovu watakapo stawi, bado wataangamizwa kwenye uharibifu wa milele.
Que cuando los perversos brotan como hierba, Y florecen todos los que hacen iniquidad, [Solo sucede] para que sean destruidos eternamente.
8 Lakini wewe, Yahwe, utatawala milele.
Pero Tú, oh Yavé, eres altísimo para siempre.
9 Hakika, watazame adui zako, Yahwe! Hakika, watazame adui zako. Wataangamia! Wale wote watendao maovu watatawanywa.
Porque ya veo que tus enemigos, oh Yavé, Ya veo que tus enemigos perecen. Son dispersados todos los obradores de iniquidad.
10 Wewe umeyainua mapembe yangu kama mapembe ya Nyati wa porini; nimepakwa mafuta safi.
Pero Tú aumentarás mi fuerza como la del búfalo. Seré ungido con aceite fresco.
11 Macho yangu yameona kuanguka kwa adui zangu; masikio yangu yamesikia maangamizi ya maadui zangu waovu.
Y mis ojos mirarán por encima de mis enemigos. Mis oídos escucharán Con respecto a los perversos que se levantan contra mí.
12 Wenye haki watastawi kama mtende; watakua kama mwerezi wa Lebanoni.
El justo florecerá como la palmera. Crecerá como un cedro en el Líbano.
13 Wamepandwa katika nyumba ya Yahwe; wakistawi katika nyua za Mungu wetu.
Plantados en la Casa de Yavé, Florecerán en los patios de nuestro ʼElohim.
14 Wao huzaa matunda hata uzeeni; hukaa safi na wenye afya,
Aun en la vejez darán fruto. Estarán llenos de savia y muy verdes
15 kutangaza kuwa Yahwe ni wa haki. Yeye ni mwamba wangu, na hakuna udhalimu ndani yake.
Para manifestar que Yavé es recto. Mi Roca es. En Él no hay injusticia.

< Zaburi 92 >