< Zaburi 91 >

1 Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
You whose home is the shelter of God Most High, whose abode is the shadow of God Almighty,
2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
can say to the Lord, “My refuge, my fortress, my God, in whom I trust.”
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
For he saves you from fowler’s snare, from deadly plague,
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
he shelters you with his pinions, and under his wings you can hide. His truth will be a shield and buckler.
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
You need not fear the terror of night, nor the arrow that flies by day,
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
nor the plague that stalks in darkness, nor the pestilence raging at noon.
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
A thousand may fall at your side, ten thousand at your right hand: but it will not draw near to you.
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
You will only look on with your eyes, and see how the wicked are punished.
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
You have made the Lord your refuge, you have made the Most High your defence.
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
You will never be met by misfortune, no plague will come near your tent,
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
for he orders his angels to guard you, wherever you go.
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
They will carry you with their hands, so you don’t hurt your foot on a stone.
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
You will trample down lions and snakes, tread on young lions and cobras.
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
“Because of their love for me, I will deliver them, I will protect those who trust my name.
15 Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
I will answer their cry and be with them in trouble, bringing them forth into safety and honor.
16 Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.
I will give them a life of many days, I will show them my salvation.”

< Zaburi 91 >