< Zaburi 91 >

1 Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
He who dwells in the secret place of the Most High will rest in the shadow of Shaddai.
2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
I will say of Jehovah, "He is my refuge and my fortress; my God, in whom I trust."
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
For he will deliver you from the snare of the fowler, and from the deadly pestilence.
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
He will cover you with his feathers. Under his wings you will take refuge. His truth is an encompassing shield.
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
You shall not be afraid of the terror by night, nor of the arrow that flies by day;
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
nor of the pestilence that walks in darkness, nor of the destruction that wastes at noonday.
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
A thousand may fall at your side, and ten thousand at your right hand; but it will not come near you.
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
You will only look with your eyes, and see the recompense of the wicked.
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
Because you have made Jehovah your refuge, and the Most High your dwelling place,
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
no evil shall overtake you; no plague shall come near your dwelling.
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
For he will put his angels in charge of you, to guard you in all your ways.
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
In their hands they will lift you up, so that you will not strike your foot against a stone.
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
You will tread upon the lion and the viper. You will trample the young lion and the serpent underfoot.
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
"Because he has set his love on me, therefore I will deliver him. I will set him on high, because he has known my name.
15 Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
He will call on me, and I will answer him. I will be with him in trouble. I will deliver him, and honor him.
16 Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.
I will satisfy him with long life, and show him my salvation."

< Zaburi 91 >