< Zaburi 91 >

1 Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
Praise of a Song, by David. He that dwells in the help of the Highest, shall sojourn under the shelter of the God of heaven.
2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
He shall say to the Lord, You are my helper and my refuge: my God; I will hope in him.
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
For he shall deliver you from the snare of the hunters, from [every] troublesome matter.
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
He shall overshadow you with his shoulders, and you shall trust under his wings: his truth shall cover you with a shield.
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
You shall not be afraid of terror by night; nor of the arrow flying by day;
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
[nor] of the [evil] thing that walks in darkness; [nor] of calamity, and the evil spirit at noon-day.
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
A thousand shall fall at your side, and ten thousand at your right hand; but it shall not come near you.
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
Only with your eyes shall you observe and see the reward of sinners.
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
For you, O Lord, are my hope: you, my soul, have made the Most High your refuge.
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
No evils shall come upon you, and no scourge shall draw near to your dwelling.
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
For he shall give his angels charge concerning you, to keep you in all your ways.
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
They shall bear you up on their hands, lest at any time you dash your foot against a stone.
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
You shall tread on the asp and basilisk: and you shall trample on the lion and dragon.
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
For he has hoped in me, and I will deliver him: I will protect him, because he has known my name.
15 Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
He shall call upon me, and I will listen to him: I am with him in affliction; and I will deliver him, and glorify him.
16 Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.
I will satisfy him with length of days, and show him my salvation.

< Zaburi 91 >