< Zaburi 88 >

1 Yahwe, Mungu wa wokovu wangu, ninalia mchana na usiku mbele zako.
[A Song. A Psalm by the sons of Korah. For the Chief Musician. To the tune of "The Suffering of Affliction." A contemplation by Heman, the Ezrahite.] Jehovah, the God of my salvation, I have cried day and night before you.
2 Sikiliza maombi yangu; utazame kulia kwangu.
Let my prayer enter into your presence. Turn your ear to my cry.
3 Maana nimejawa taabu, na uhai wangu umefika kuzimuni. (Sheol h7585)
For my soul is full of troubles. My life draws near to Sheol. (Sheol h7585)
4 Watu hunichukulia kama wale waendao chini shimoni; mimi ni mtu asiye na nguvu.
I am counted among those who go down into the pit. I am like a man who has no help,
5 Nimetelekezwa miongoni mwa wafu; niko kama mfu alalaye katika kaburi, wao ambao wewe huwajari tena kwa sababu wametengwa mbali na nguvu zako.
set apart among the dead, like the slain who lie in the grave, whom you remember no more. They are cut off from your hand.
6 Wewe umeniweka katika sehemu ya chini kabisa ya shimo, sehemu yenye giza na kilindini.
You have laid me in the lowest pit, in the darkest depths.
7 Gadhabu yako yanielemea, na mawimbi yako yote yanatua juu yangu. (Selah)
Your wrath lies heavily on me. You have afflicted me with all your waves. (Selah)
8 Kwa sababu yako, wale wanijuao wote hunikwepa. Umenifanya wakutisha machoni pao. Nimefungwa na siwezi kutoroka.
You have taken my friends from me. You have made me an abomination to them. I am confined, and I can't escape.
9 Macho yangu yamefifia kutokana na shida; kila siku nakuita wewe, Yahwe; ninakunyoshea wewe mikono yangu.
My eyes are dim from grief. I have called on you daily, Jehovah. I have spread out my hands to you.
10 Je! utafanya miujiza kwa ajili ya wafu? Wale waliokufa watafufuka na kukusifu wewe? (Selah)
Do you show wonders to the dead? Do the dead rise up and praise you? (Selah)
11 Uaminifu wa agano lako utatangazwa kaburini? au uaminifu wako mahali pa wafu?
Is your loving kindness declared in the grave? Or your faithfulness in Destruction?
12 Matendo yako ya ajabu yatajulikana gizani? au haki yako katika mahali pa usahaulifu?
Are your wonders made known in the dark? Or your righteousness in the land of forgetfulness?
13 Lakini ninakulilia wewe, Yahwe; wakati wa asubuhi maombi yangu huja kwako.
But to you, Jehovah, I have cried. In the morning, my prayer comes before you.
14 Yahwe, kwa nini unanikataa? Kwa nini unauficha uso wako mbali nami?
Jehovah, why do you reject my soul? Why do you hide your face from me?
15 Nimekuwa nikiteswa kila siku na hatihati ya kifo tangu ujana wangu. Nimeteseka dhidi ya hofu yako kuu; ninakata tamaa.
I am afflicted and ready to die from my youth up. While I suffer your terrors, I am distracted.
16 Matendo yako ya hasira yamepita juu yangu, na matendo yako ya kutisha yameniangamiza.
Your fierce wrath has gone over me. Your terrors have cut me off.
17 Siku zote yananizingira mimi kama maji; yote yamenizunguka mimi.
They came around me like water all day long. They completely engulfed me.
18 Wewe umemuondoa kwangu kila rafiki na anijuaye. Na sasa anijuaye pekee ni giza.
You have put lover and friend far from me, and my friends into darkness.

< Zaburi 88 >