< Zaburi 85 >

1 Yahwe, wewe umeonesha fadhilia kwenye nchi yako; umeurejesha ustawi wa Yakobo.
Para él maestro de coro. De los hijos de Coré. Salmo. Oh Yahvé, has sido propicio a tu tierra, has trocado en bien la suerte de Jacob.
2 Umesamehe dhambi ya watu wako; umezisitiri dhambi zao zote. (Selah)
Has quitado la iniquidad de tu pueblo, cubierto todos sus pecados.
3 Umeondoa ghadhabu yako yote; umeiacha hasira yako kali.
Has puesto fin a todo tu resentimiento, desistido del furor de tu ira.
4 Uturejeshe sisi, Ee Mungu wa wokovu wetu, na uikomeshe chuki yako juu yetu.
Restáuranos, oh Dios, Salvador nuestro; aparta de nosotros tu indignación.
5 Je! Utaendelea kuwa na hasira juu yetu milele? utadumisha hasira kizazi chote kijacho?
¿Acaso estarás siempre enojado con nosotros? ¿Extenderás tu saña de generación en generación?
6 Je, hautatuhuisha tena? Kisha watu wako watafurahia katika wewe.
¿No volverás Tú a darnos vida, para que tu pueblo se alegre en Ti?
7 Utuoneshe sisi uaminifu wa agano lako, Yahwe, utupe sisi wokovu wako.
Muéstranos, Yahvé, tu misericordia y envíanos tu salvación.
8 Nitasikiliza yale Yahwe Mungu asemayo, maana yeye atafanya amani pamoja na watu wake, wafuasi wake waminifu. Lakini lazima wasirudi tena katika njia za kipumbavu.
Quiero escuchar lo que dirá Yahvé mi Dios; sus palabras serán de paz para su pueblo y para sus santos, y para los que de corazón se vuelvan a Él.
9 Hakika wokovu wake u karibu na wale wanao mwabudu yeye; kisha utukufu utabaki katika nchi yetu.
Sí, cercana está su salvación para los que le temen; y la Gloria fijará su morada en nuestro país.
10 Uaminifu wa agano na uaminifu vimekutana pamoja; haki na amani vimebusiana.
La misericordia y la fidelidad se saldrán al encuentro; se darán el ósculo la justicia y la paz.
11 Uaminifu unatoa chemchem kutoka ardhini, na haki hutazama chini kutoka mawinguni.
La fidelidad germinará de la tierra y la justicia se asomará desde el cielo.
12 Ndiyo, Yahwe atatoa baraka zake njema, na nchi itatoa mazao yake.
El mismo Yahvé dará el bien y nuestra tierra dará su fruto.
13 Haki itaenda mbele zake na kufanya njia kwa ajili ya nyayo zake.
La justicia marchará ante Él y la salud sobre la huella de sus pasos.

< Zaburi 85 >