< Zaburi 83 >

1 Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
Una canción. Un salmo de Asaf. Dios, no guardes silencio. No te quedes callado, y no te quedes quieto, Dios.
2 Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
Porque, he aquí, tus enemigos están agitados. Los que te odian han levantado la cabeza.
3 Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
Conspiran con astucia contra tu pueblo. Conspiran contra tus seres queridos.
4 “Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
“Vamos”, dicen, “destruyámoslos como nación, para que el nombre de Israel no sea más recordado”.
5 Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
Porque han conspirado juntos con una sola mente. Forman una alianza contra ti.
6 Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
Las tiendas de Edom y de los ismaelitas; Moab, y los Hagritas;
7 Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
Gebal, Amón y Amalec; Filistea con los habitantes de Tiro;
8 Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
También Asiria se une a ellos. Han ayudado a los hijos de Lot. (Selah)
9 Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
Haz con ellos lo que hiciste con Madián, como a Sísara, como a Jabín, en el río Cisón;
10 Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
que perecieron en Endor, que se convirtió en estiércol para la tierra.
11 Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
Haz que sus nobles sean como Oreb y Zeeb, sí, todos sus príncipes como Zebah y Zalmunna,
12 Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
que dijo: “Tomemos posesión de las tierras de pastoreo de Dios”.
13 Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
Dios mío, haz que sean como una planta rodadora, como paja ante el viento.
14 Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
Como el fuego que quema el bosque, como la llama que incendia las montañas,
15 Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
así que persíguelos con tu tempestad, y aterrorízalos con tu tormenta.
16 Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
Llena sus rostros de confusión, para que busquen tu nombre, Yahvé.
17 Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
Que queden desilusionados y consternados para siempre. Sí, que se confundan y perezcan;
18 Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.
para que sepan que sólo tú, cuyo nombre es Yahvé, eres el Altísimo sobre toda la tierra.

< Zaburi 83 >