< Zaburi 80 >

1 Usikie, Mchungaji wa Israel, wewe uliye muongoza Yusufu kama kundi; wewe uketiye juu ya makerubi, utuangazie!
[For the Chief Musician. To the tune of "The Lilies of the Covenant." A Psalm by Asaph.] Hear us, Shepherd of Israel, you who lead Joseph like a flock, you who sit above the cherubim, shine forth.
2 Machoni pa Efraimu na Benjamini na Manase, uziinue nguvu zako; njoo na utuokoe.
Before Ephraim and Benjamin and Manasseh, stir up your might. Come to save us.
3 Mungu, uturejeshe sisi; uangaze uso wako juu yetu, nasi tutaokolewa.
Restore us, God. Cause your face to shine, and we will be saved.
4 Yahwe Mungu wa majeshi, mpaka lini utawakasirikia watu wako wanapoomba?
Jehovah, the God of hosts, How long will you be angry against the prayer of your people?
5 Umewalisha wa mkate wa machozi na umewapa machozi ili wanywe katika kiasi kikubwa.
You have fed them with the bread of tears, and given them tears to drink in large measure.
6 Umetufanya kitu kwa ajili ya majirani zetu kubishania, na maadui zetu hucheka kuhusu sisi kati yao.
You make us a source of contention to our neighbors. Our enemies have mocked us.
7 Mungu wa majeshi, uturejeshe sisi; nasi tutaokolewa.
Restore us, God of hosts. Cause your face to shine, and we will be saved.
8 Wewe ulileta mzabibu kutoka Misri; ukawafukuza mataifa na ukaupanda.
You brought a vine out of Egypt. You drove out the nations, and planted it.
9 Uliisafisha ardhi kwa ajil yake; nao ulipata mzizi na kuijaza nchi.
You cleared the ground for it. It took deep root, and filled the land.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, mierezi ya Mungu kwa matawi yake.
The mountains were covered with its shadow. Its boughs were like God's cedars.
11 Ilieneza matawi yake mbali kama bahari na mashina yake mpaka kwenye Mto Euphrates.
It sent out its branches to the sea, Its shoots to the River.
12 Kwa nini umezibomoa kuta zake hata wapitao karibu huyachuma matunda yake.
Why have you broken down its walls, so that all those who pass by the way pluck it?
13 Ngurue wa msituni wanauharibu, na wanyama wa kondeni wanaula.
The boar out of the wood ravages it. The wild animals of the field feed on it.
14 Urudi, Ee Mungu wa majeshi; kutoka mbinguni utazame chini na uuangalie na kuujali huu mzabibu.
Return, we beg you, God of hosts. Look down from heaven, and see, and visit this vine,
15 Huu ni mzizi ambao mkono wako wa kuume umeupanda, mashina ambayo wewe uliyafanya yakue.
the stock which your right hand planted, the branch that you made strong for yourself.
16 Yamekatwa na kuchomwa; yameangamia kwa sababu ya kukemea kwako.
It's burned with fire. It's cut down. They perish at your rebuke.
17 Mkono wako na uwe juu ya mtu aliye mkono wako wa kuume, kwa mwana wa mtu uliyemfanya imara kwa ajili yako mwenyewe.
Let your hand be on the man of your right hand, on the son of man whom you made strong for yourself.
18 Ndipo hatuta kuacha wewe; utuhuishe, nasi tutaliita jina lako.
So we will not turn away from you. Revive us, and we will call on your name.
19 Yahwe, Mungu wa majeshi, uturejeshe sisi; utuangazie nuru ya uso wako, nasi tutaokolewa.
Restore us, Jehovah, the God of hosts. Cause your face to shine, and we will be saved.

< Zaburi 80 >