< Zaburi 80 >

1 Usikie, Mchungaji wa Israel, wewe uliye muongoza Yusufu kama kundi; wewe uketiye juu ya makerubi, utuangazie!
For the Leader; upon Shoshannim. A testimony. A Psalm of Asaph. Give ear, O Shepherd of Israel, Thou that leadest Joseph like a flock; Thou that art enthroned upon the cherubim, shine forth.
2 Machoni pa Efraimu na Benjamini na Manase, uziinue nguvu zako; njoo na utuokoe.
Before Ephraim and Benjamin and Manasseh, stir up Thy might, and come to save us.
3 Mungu, uturejeshe sisi; uangaze uso wako juu yetu, nasi tutaokolewa.
O God, restore us; and cause Thy face to shine, and we shall be saved.
4 Yahwe Mungu wa majeshi, mpaka lini utawakasirikia watu wako wanapoomba?
O LORD God of hosts, how long wilt Thou be angry against the prayer of Thy people?
5 Umewalisha wa mkate wa machozi na umewapa machozi ili wanywe katika kiasi kikubwa.
Thou hast fed them with the bread of tears, and given them tears to drink in large measure.
6 Umetufanya kitu kwa ajili ya majirani zetu kubishania, na maadui zetu hucheka kuhusu sisi kati yao.
Thou makest us a strife unto our neighbours; and our enemies mock as they please.
7 Mungu wa majeshi, uturejeshe sisi; nasi tutaokolewa.
O God of hosts, restore us; and cause Thy face to shine, and we shall be saved.
8 Wewe ulileta mzabibu kutoka Misri; ukawafukuza mataifa na ukaupanda.
Thou didst pluck up a vine out of Egypt; Thou didst drive out the nations, and didst plant it.
9 Uliisafisha ardhi kwa ajil yake; nao ulipata mzizi na kuijaza nchi.
Thou didst clear a place before it, and it took deep root, and filled the land.
10 Milima ilifunikwa kwa kivuli chake, mierezi ya Mungu kwa matawi yake.
The mountains were covered with the shadow of it, and the mighty cedars with the boughs thereof.
11 Ilieneza matawi yake mbali kama bahari na mashina yake mpaka kwenye Mto Euphrates.
She sent out her branches unto the sea, and her shoots unto the River.
12 Kwa nini umezibomoa kuta zake hata wapitao karibu huyachuma matunda yake.
Why hast Thou broken down her fences, so that all they that pass by the way do pluck her?
13 Ngurue wa msituni wanauharibu, na wanyama wa kondeni wanaula.
The boar out of the wood doth ravage it, that which moveth in the field feedeth on it.
14 Urudi, Ee Mungu wa majeshi; kutoka mbinguni utazame chini na uuangalie na kuujali huu mzabibu.
O God of hosts, return, we beseech Thee; look from heaven, and behold, and be mindful of this vine,
15 Huu ni mzizi ambao mkono wako wa kuume umeupanda, mashina ambayo wewe uliyafanya yakue.
And of the stock which Thy right hand hath planted, and the branch that Thou madest strong for Thyself.
16 Yamekatwa na kuchomwa; yameangamia kwa sababu ya kukemea kwako.
It is burned with fire, it is cut down; they perish at the rebuke of Thy countenance.
17 Mkono wako na uwe juu ya mtu aliye mkono wako wa kuume, kwa mwana wa mtu uliyemfanya imara kwa ajili yako mwenyewe.
Let Thy hand be upon the man of Thy right hand, upon the son of man whom Thou madest strong for Thyself.
18 Ndipo hatuta kuacha wewe; utuhuishe, nasi tutaliita jina lako.
So shall we not turn back from Thee; quicken Thou us, and we will call upon Thy name.
19 Yahwe, Mungu wa majeshi, uturejeshe sisi; utuangazie nuru ya uso wako, nasi tutaokolewa.
O LORD God of hosts, restore us; cause Thy face to shine, and we shall be saved.

< Zaburi 80 >