< Zaburi 79 >

1 Zaburi ya Asafu. Mungu, Mataifa ya kigeni yameingia kwenye urithi wako; wamelinajisi hekalu lako takatifu; wameigeuza Yerusalemu kuwa chungu cha magofu.
Psalm Asafu. O Bog, prišli so narodi v posestvo tvoje, oskrunili so hram svetosti tvoje, v groblje izpremenili so Jeruzalem.
2 Wamezitoa maiti za watumishi wako ziwe chakula cha ndege wa angani, miili ya watakatifu wako iwe chakula cha wanyama wa nchi.
Dali so hlapcev tvojih truplo za hrano tičem nebeškim; meso njih, katerim si milosten, zemeljskim zverém.
3 Wamemwaga damu zao kama maji sehemu zote za Yesrusalemu, na hakuwepo wa kuwazika.
Prelivali so kri njihovo kakor vodo okrog Jeruzalema, in ni ga bilo, da bi pokopaval.
4 Sisi tumekuwa aibu kwa majirani zetu, tukidhihakiwa na kuzomewa na wale wanaotuzunguka.
V zasramovanje smo sosedom našim, v zasmehovanje in norčevanje njim, kateri so okolo nas.
5 Mpaka lini Yahwe? Utabaki kuwa na hasira milele? Ni kwa muda gani hasira yako ya wivu itawaka kama moto?
Doklej, Gospod? bodeš-li jezil se večno? bode li gorela kakor ogenj gorečnost tvoja?
6 Mwaga hasira yako juu ya mataifa ambayo hayakujui wewe na ufalme ambao hauliiti jina lako.
Izlij srd svoj nad one narode, kateri te ne spoznavajo, in nad kraljestva, katera ne kličejo tvojega imena.
7 Kwa maana walimvamia Yakobo na waliharibu kijiji chake.
Ker pojedli so Jakoba, in razdejali so prebivališče njegovo.
8 Usiendelee kukumbuka dhambi za baba zetu dhidi yetu; matendo yako ya huruma yaje kwetu, maana tuko chini.
Ne spomínjaj se zoper nas krivic preteklih časov, hiti naj in prehití nas usmiljenje tvoje, ker obožali smo silno.
9 Utusaidie, Mungu wa wokovu wetu, kwa ajili ya utukufu wa jina lako; utuokoe na usamehe dhambi zetu kwa ajili ya jina lako.
Pomagaj nam, Bog, blaginje naše, zavoljo česti svojega imena, in reši nas ter prizanesi nam grehe naše zavoljo svojega imena.
10 Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Mungu wao yuko wapi?” Damu ya watumishi wako ambayo ilimwagwa na ilipize kisasi juu ya mataifa mbele ya macho yako.
Zakaj naj bi govorili oni narodi: "Kje je njih Bog?" Znano bodi med onimi narodi pred našimi očmi maščevanje krvi prelite hlapcev tvojih.
11 Kilio cha wafungwa na kije mbele zako; kwa uweza wa nguvu zako uwaweke ai wana wa mauti.
Pred obličje tvoje naj pride zdihovanje jetnika, po velikosti roke svoje stóri, da ostanejo, kateri se že izročajo smrti.
12 Uwalipize majirani zetu vifuani mwao mara saba zaidi ya walivyo kutukana wewe, Bwana.
Povrni torej sosedom našim sedemkrat v njih naročje sramoto njih, katero so ti delali, Gospod.
13 Hivyo sisi watu wako na kondoo wa malisho yako tutakushukuru milele. Tutazisimulia sifa zako kwa vizazi vyote.
In mi ljudstvo tvoje, in čeda paše tvoje, bodemo slavili te večno; od roda do roda bodemo oznanjali hvalo tvojo.

< Zaburi 79 >