< Zaburi 79 >

1 Zaburi ya Asafu. Mungu, Mataifa ya kigeni yameingia kwenye urithi wako; wamelinajisi hekalu lako takatifu; wameigeuza Yerusalemu kuwa chungu cha magofu.
O God, the heathen are come into your inheritance; your holy temple have they defiled; they have laid Jerusalem on heaps.
2 Wamezitoa maiti za watumishi wako ziwe chakula cha ndege wa angani, miili ya watakatifu wako iwe chakula cha wanyama wa nchi.
The dead bodies of your servants have they given to be meat to the fowls of the heaven, the flesh of your saints to the beasts of the earth.
3 Wamemwaga damu zao kama maji sehemu zote za Yesrusalemu, na hakuwepo wa kuwazika.
Their blood have they shed like water round about Jerusalem; and there was none to bury them.
4 Sisi tumekuwa aibu kwa majirani zetu, tukidhihakiwa na kuzomewa na wale wanaotuzunguka.
We are become a reproach to our neighbors, a scorn and derision to them that are round about us.
5 Mpaka lini Yahwe? Utabaki kuwa na hasira milele? Ni kwa muda gani hasira yako ya wivu itawaka kama moto?
How long, LORD? will you be angry for ever? shall your jealousy burn like fire?
6 Mwaga hasira yako juu ya mataifa ambayo hayakujui wewe na ufalme ambao hauliiti jina lako.
Pour out your wrath on the heathen that have not known you, and on the kingdoms that have not called on your name.
7 Kwa maana walimvamia Yakobo na waliharibu kijiji chake.
For they have devoured Jacob, and laid waste his dwelling place.
8 Usiendelee kukumbuka dhambi za baba zetu dhidi yetu; matendo yako ya huruma yaje kwetu, maana tuko chini.
O remember not against us former iniquities: let your tender mercies speedily prevent us: for we are brought very low.
9 Utusaidie, Mungu wa wokovu wetu, kwa ajili ya utukufu wa jina lako; utuokoe na usamehe dhambi zetu kwa ajili ya jina lako.
Help us, O God of our salvation, for the glory of your name: and deliver us, and purge away our sins, for your name’s sake.
10 Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Mungu wao yuko wapi?” Damu ya watumishi wako ambayo ilimwagwa na ilipize kisasi juu ya mataifa mbele ya macho yako.
Why should the heathen say, Where is their God? let him be known among the heathen in our sight by the revenging of the blood of your servants which is shed.
11 Kilio cha wafungwa na kije mbele zako; kwa uweza wa nguvu zako uwaweke ai wana wa mauti.
Let the sighing of the prisoner come before you; according to the greatness of your power preserve you those that are appointed to die;
12 Uwalipize majirani zetu vifuani mwao mara saba zaidi ya walivyo kutukana wewe, Bwana.
And render to our neighbors sevenfold into their bosom their reproach, with which they have reproached you, O Lord.
13 Hivyo sisi watu wako na kondoo wa malisho yako tutakushukuru milele. Tutazisimulia sifa zako kwa vizazi vyote.
So we your people and sheep of your pasture will give you thanks for ever: we will show forth your praise to all generations.

< Zaburi 79 >