< Zaburi 76 >

1 Mungu amefanya mwenyewe kujulikana katika Yuda; jina lake ni kuu katika Israeli.
Au chef de musique. Sur Neguinoth. Psaume d’Asaph. Cantique. Dieu est connu en Juda, son nom est grand en Israël;
2 Hema yake iko salemu; makao yake yako yako Sayuni.
Et son tabernacle est en Salem, et son domicile en Sion.
3 Huko ndiko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita. (Selah)
Là, il a brisé les éclairs de l’arc, le bouclier, et l’épée, et la bataille. (Sélah)
4 Wewe unang'aa sana na huufunua utukufu wako, ushukapo kutoka milimani, ambako uliwauwa mateka.
Tu es plus resplendissant, plus magnifique que les montagnes de la rapine.
5 Wenye moyo shujaa walitekwa nyara; walilala mauti. Mashujaa wote walikuwa wanyonge.
Les forts de cœur ont été dépouillés, ils ont dormi leur sommeil, et aucun des hommes vaillants n’a trouvé ses mains.
6 Kwa kukemea kwako, ewe Mungu wa Yakobo, wote gari na farasi walilala mauti.
Quand tu les as tancés, ô Dieu de Jacob! chars et chevaux se sont endormis profondément.
7 Wewe, ndiyo wewe, ni wa kuogopwa; ni nani awezaye kusimama mbele yako wakati ukiwa na hasira?
Tu es terrible, toi; et qui est-ce qui subsistera devant toi, dès que ta colère [éclate]?
8 Kutoka mbinguni wewe uliifanya hukumu yako isikike; nchi iliogopa na ikaa kimya
Tu fis entendre des cieux le jugement; la terre en eut peur, et se tint tranquille,
9 wakati wewe, Mungu, ulipoinuka kutekeleza hukumu na kuwaokoa wote wa nchi walio onewa. (Selah)
Quand tu te levas, ô Dieu, pour le jugement, pour sauver tous les débonnaires de la terre. (Sélah)
10 Hakika hukumu ya hasira yako dhidi ya binadamu itakuletea wewe sifa; wewe hujifunga mwenyewe hasira yako iliyo baki.
Car la colère de l’homme te louera; tu te ceindras du reste de la colère.
11 Wekeni nadhiri kwa Yahwe Mungu wenu na kuzihifadhi. Nao wote wamzungukao yeye mleteeni zawadi yeye ambaye ni wa kuogopwa.
Vouez, et acquittez [vos vœux] envers l’Éternel, votre Dieu; que tous ceux qui l’entourent apportent des présents au Redoutable.
12 Yeye huzikata roho za wakuu; huogopwa na wafalme wa nchi.
Il retranchera l’esprit des princes, il est terrible aux rois de la terre.

< Zaburi 76 >