< Zaburi 76 >

1 Mungu amefanya mwenyewe kujulikana katika Yuda; jina lake ni kuu katika Israeli.
In Judah [Praised], God is known. His name is great in Israel [God prevails].
2 Hema yake iko salemu; makao yake yako yako Sayuni.
His tabernacle is also in Salem [Complete peace, Perfect peace]; His dwelling place in Zion [Mountain ridge, Marking].
3 Huko ndiko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita. (Selah)
There he broke the flaming arrows of the bow, the shield, and the sword, and the weapons of war. (Selah) ·contemplation with musical interlude·.
4 Wewe unang'aa sana na huufunua utukufu wako, ushukapo kutoka milimani, ambako uliwauwa mateka.
Glorious are you, and excellent, more than mountains of game.
5 Wenye moyo shujaa walitekwa nyara; walilala mauti. Mashujaa wote walikuwa wanyonge.
Valiant men lie plundered, they have slept their last sleep. None of the men of war can lift their hands.
6 Kwa kukemea kwako, ewe Mungu wa Yakobo, wote gari na farasi walilala mauti.
At your rebuke, God of Jacob [Supplanter], both chariot and horse are cast into a deep sleep.
7 Wewe, ndiyo wewe, ni wa kuogopwa; ni nani awezaye kusimama mbele yako wakati ukiwa na hasira?
You, even you, are to be feared. Who can stand in your sight when you are angry?
8 Kutoka mbinguni wewe uliifanya hukumu yako isikike; nchi iliogopa na ikaa kimya
You pronounced judgment to be sh'ma ·heard obeyed· from heaven. The earth feared, and was silent,
9 wakati wewe, Mungu, ulipoinuka kutekeleza hukumu na kuwaokoa wote wa nchi walio onewa. (Selah)
when God arose to judgment, to save all the afflicted ones of the earth. (Selah) ·contemplation with musical interlude·.
10 Hakika hukumu ya hasira yako dhidi ya binadamu itakuletea wewe sifa; wewe hujifunga mwenyewe hasira yako iliyo baki.
Surely the wrath of man yadah ·extend hands in thankful praise· to you. The survivors of your wrath are restrained.
11 Wekeni nadhiri kwa Yahwe Mungu wenu na kuzihifadhi. Nao wote wamzungukao yeye mleteeni zawadi yeye ambaye ni wa kuogopwa.
Make vows to Adonai your God, and fulfill them! Let all of his neighbors bring presents to him who is to be feared.
12 Yeye huzikata roho za wakuu; huogopwa na wafalme wa nchi.
He will cut off the spirit of princes. He is feared by the kings of the earth.

< Zaburi 76 >