< Zaburi 75 >

1 Tunatoa shukrani kwako, Mungu; tunatoa shukrani, maana wewe unaufunua uwepo wako; watu huzungumza kuhusu kazi zako za ajabu.
To the choirmaster al-tashcheth a psalm of Asaph a song. We give thanks to you - O God we give thanks and [is] near name your people recount wonders your.
2 Kwa wakati maalum nitahukumu kwa haki.
If I will take an appointed time I uprightness I will judge.
3 Ingawa nchi na wenyeji wote watatikisika katika hofu, ninaifanyia nchi nguzo za kutosha. (Selah)
[are] melting away [the] earth And all inhabitants its I I put in order pillars its (Selah)
4 Nilisema kwa wenye kiburi, “Msiwe wenye kiburi,” na kwa waovu, “Msiinue mapembe.
I say to the boasters may not you boast and to the wicked [people] may not you lift up a horn.
5 Msiinue mapembe yenu kwenye marefu; wala msizungumze kwa shingo ya kiburi.”
May not you lift up to the height horn your may you speak with a neck arrogance.
6 Sio kutoka mashariki au magharibi, na wala sio kutoka jangwani ambako kuinuliwa kunakuja.
For not [is] from [the] going out and from [the] setting place and not from [the] wilderness exaltation.
7 Bali Mungu ni muhumkumu; humshusha huyu na kumuinua huyu.
For God [is the] judge this one he brings low and this one he lifts up.
8 Kwa kuwa Yahwe kashikilia mkononi mwake kikombe cha mvinyo wenye povu, ambao umechanganywa na vilolezo, naye huimimina. Hakika waovu wote wa duniani watakunywa mvinyo hadi tone la mwisho.
For a cup [is] in [the] hand of Yahweh and wine it is foaming - full spiced drink and he has poured out some of this surely dregs its they will drain they will drink all [the] wicked [people] of [the] earth.
9 Bali mimi nitaendelea kusema yale ambayo umeyatenda; nami nitamwimbia sifa Mungu wa Yakobo.
And I I will declare for ever I will sing praises to [the] God of Jacob.
10 Yeye husema, “Nitayakata mapembe yote ya waovu, lakini mapembe ya wenye haki yatainuliwa.”
And all [the] horns of wicked [people] I will cut off they will be lifted up [the] horns of [the] righteous.

< Zaburi 75 >