< Zaburi 73 >

1 Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio na moyo safi.
Psalm Asafov. Dá, dober je Bog Izraelu, čistim v srci.
2 Lakini kwangu mimi, kidogo tu miguu yangu iteleze; miguu yangu karibu iteleze kutoka kwangu
Jaz pa, malo da se niso izpotaknile noge moje, skoraj nič, da niso izpodrsnili koraki moji,
3 kwa sababu niliwaonea wivu wenye kiburi nilipoona mafanikio ya waovu.
Ko sem zavidal blazne, gledal krivičnih blagostanje,
4 Kwa maana hawana maumivu hadi kufa kwao, lakini wana nguvu na wameshiba.
Ker ni ga vozla notri do njih smrti, temuč tolsta je njih moč.
5 Wako huru dhidi ya mizigo ya watu wengine; nao hawateswi kama watu wengine.
V trudu človeškem niso, in z drugimi ljudmi ne tepó jih nadloge.
6 Kiburi kinawapamba kama mkufu kwenye shingo zao; jeuri huwavika kama vazi.
Zatorej jih obdajajo prevzetnosti verige, pokriva jih kakor dika silovitost.
7 Katika upofu wa jinsi hii dhambi huja; mawazo maovu hupita mioyoni mwao.
Svétiti se jim od tolšče obé očesi, kipé misli srčne.
8 Wao hudhihaki na kuongea kwa namna ya uovu; kwa kiburi chao hutishia mateso.
Kužni so, in hudobno govoré zatiranje, in z višave govoré.
9 Wameweka vinywa vyao dhidi ya mbingu, na ndimi zao hutanga tanga duniani.
V nebo dvigajo usta svoja, in jezik njih prehaja zemljo.
10 Kwa hiyo watu wake huwageukia na maji yaliyojaa hukaushwa.
Zatorej se vrača sem ljudstvo njegovo, ko se čaše, vode polne, iztiskajo jim,
11 Nao husema, “Mungu anajuaje? Yako maarifa kwake yeye aliye juu?”
Da pravijo: Kako bi poznal Bog mogočni? ali bi bilo znanje v višavi?
12 Fahamu: watu hawa ni waovu; mara zote hawajali, wakifanyika matajiri na matajiri.
Glej tiste krivične, kako mirni vekomaj množijo močí.
13 Hakika nimeutunza moyo wangu bure na nimenawa mikono yangu pasipo kukosa.
Vendar zastonj čistim svoje srce, in v snagi umivam rok svoje;
14 Maana mchana kutwa nimeteswa na kuadhibiwa kila asubuhi.
Ko me tepe vsak dan, in pokora moja mi je gotova vsako jutro.
15 Kama ningesema, “Ningesema mambo haya,” kumbe nigewasaliti kizazi hiki cha watoto wenu.
Ako rečem: Pravil bodem to; glej, izdajalec bi bil zarodu tvojih sinov.
16 Ingawa nilijaribu kuyaelewa mambo haya, yalikuwa ni magumu sana kwangu.
Ako bi mislil spoznati to, težavno se mi je zdelo v mojih očéh;
17 Ndipo nilipoingia patakatifu pa Mungu na kuelewa hatma yao.
Dokler sem stopil v svetišča Boga mogočnega, zagledal njih konec.
18 Hakika wewe huwaweka penye utelezi; huwaangusha mpaka palipoharibika.
Ali na polzlo jih staviš, mečeš jih dol v podrtije.
19 Jinsi gani wamekuwa ukiwa kwa muda mfupi! Wamefika mwisho nao wamemaliza kwa utisho.
Kako ginejo v zapuščenost, kakor v hipu minejo, konec jih je v grozah.
20 Wao ni kama ndoto wakati wa mtu kuamka; Bwana, utakapo inuka, utazidharau ndoto zao.
Kakor sanje, ko se je zbudil kdo: Bog, ko se zbudiš, zaničuješ njih podobo.
21 Maana moyo wangu ulipata uchungu, nami nilijeruhiwa sana.
Ko se razdraži srce moje, in ko sem se v ledvicah svojih samega zbadal,
22 Nilikuwa mjinga na sijui neno; nilikuwa kama mnyama tu mbele yako.
Tedaj sem bil brezpameten, ko nisem vedel: kakor živina bil sem pri tebi.
23 Lakini mimi nipo pamoja nawe daima; umenishika mkono wa kuume.
Zatorej bodem jaz vedno s teboj; prijel si roko desno mojo.
24 Utaniongoza kwa shauri lako na baadaye utanipokea katika utukufu.
Sè sovetom svojim me spremljaj, da me potem v slavo sprejmeš.
25 Ni nani niliye naye mbinguni isipokuwa wewe? Hakuna nimtamaniye duniani isipokuwa wewe.
Kdo bi mi bil v nebesih razen tebe? in razen tebe se nikogar ne veselim na zemlji.
26 Mwili wangu na moyo wangu huwa dhaifu, bali Mungu ndiye nguvu ya moyo wangu daima.
Ko peša meso moje in srce moje, skala srca mojega in delež moj je Bog vekomaj.
27 Wale walio mbali nawe wataangamia; utawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
Ker glej, kateri so daleč od tebe, ginejo; pokončaš ga, kdor koli se s prešestvovanjem izneveri tebi.
28 Lakini mimi, linipasalo kufanya ni kumkaribia Mungu. Nimemfanya Bwana Yahwe kimbilio langu. Nami nitayatangaza matendo yako yote.
Meni torej je dobro, da sem blizu Bogu; v Gospoda stavim svoje pribežališče, da oznanjam vsa dela tvoja.

< Zaburi 73 >