< Zaburi 69 >

1 Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
Save me, God, for the waters have come up to my neck!
2 Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
I sink in deep mire, where there is no foothold. I have come into deep waters, where the floods overflow me.
3 Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
I am weary with my crying. My throat is dry. My eyes fail, looking for my God.
4 Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
Those who hate me without a cause are more than the hairs of my head. Those who want to cut me off, being my enemies wrongfully, are mighty. I am forced to restore what I didn’t steal.
5 Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
God, you know my foolishness. My sins are not hidden from you.
6 Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
Don’t let those who wait for you be shamed through me, Lord Adonai Tzva'ot [Yahweh Commander of heaven’s armies]. Don’t let those who seek you be brought to dishonor through me, God of Israel [God prevails].
7 Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
Because for your sake, I have borne reproach. Shame has covered my face.
8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
I have become a stranger to my brothers, an alien to my mother’s children.
9 Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
For the zeal of your house consumes me. The insults of those insulting you have fallen on me.
10 Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
When I wept and I fasted, that was to my reproach.
11 Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
When I made sackcloth my clothing, I became a byword to them.
12 Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
Those who sit in the gate talk about me. I am the song of the drunkards.
13 Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
But as for me, my prayer is to you, Adonai, in an acceptable time. God, in the abundance of your loving kindness, answer me in the truth of your yesha' ·salvation·.
14 Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
Deliver me out of the mire, and don’t let me sink. Let me be delivered from those who hate me, and out of the deep waters.
15 Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
Don’t let the flood waters overwhelm me, neither let the deep swallow me up. Don’t let the pit shut its mouth on me.
16 Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
Answer me, Adonai, for your cheshed ·loving-kindness· is good. According to the multitude of your tender racham · merciful love·, turn to me.
17 Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
Don’t hide your face from your servant, for I am in distress. Answer me speedily!
18 Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
Draw near to my soul, and redeem it. Ransom me because of my enemies.
19 Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
You know my reproach, my shame, and my dishonor. My adversaries are all before you.
20 Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
Reproach has broken my heart, and I am full of heaviness. I looked for some to take pity, but there was none; for comforters, but I found none.
21 Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
They also gave me gall for my food. In my thirst, they gave me vinegar to drink.
22 Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
Let their table before them become a snare. May it become a retribution and a trap.
23 Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
Let their eyes be darkened, so that they can’t see. Let their backs be continually bent.
24 Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
Pour out your indignation on them. Let the fierceness of your anger overtake them.
25 Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
Let their habitation be desolate. Let no one dwell in their tents.
26 Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
For they persecute him whom you have wounded. They tell of the sorrow of those whom you have hurt.
27 Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
Charge them with crime upon crime. Don’t let them come into your righteousness.
28 Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
Let them be blotted out of the book of life, and not be written with the upright.
29 Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
But I am in pain and distress. Let your yishu'ah ·salvation·, O God, protect me.
30 Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
I will praise the name of God with a song, and will magnify him with thanksgiving.
31 Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
It will please Adonai better than an ox, or a bull that has horns and hoofs.
32 Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
The humble have seen it, and are glad. You who seek after God, let your heart live.
33 Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
For Adonai sh'ma ·hears obeys· the needy, and does not despise his captive people.
34 Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
Let heaven and earth praise him; the seas, and everything that moves therein!
35 Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
For God will save Zion [Mountain ridge, Marking], and build the cities of Judah [Praised]. They shall settle there, and own it.
36 Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.
The children also of his servants shall inherit it. Those who 'ahav ·affectionately love· his name shall dwell therein.

< Zaburi 69 >