< Zaburi 68 >

1 Mungu ainuke, maadui zake watawanyike; pia wale wamchukiao wakimbie mbele zake.
For the leader. Of David. A psalm. A song. God arises, his enemies scatter: they who hate him flee before him.
2 Kama moshi uondoshwavyo, hivyo uwaondoshe wao; kama nta iyeyukavo mbele ya moto, hivyo waovu waangamizwe uweponi mwa Mungu.
As smoke before wind is driven, as wax melts before fire, so before God vanish the wicked.
3 Bali wenye haki wafurahi; washangilie mbele za Mungu; washangilie na kufurahi.
But the righteous rejoice in God’s presence, they exult with exceeding joy.
4 Mwimbieni Mungu! Lisifuni jina lake! Msifuni yule aendeshaye farasi kwenye tambarare ya bonde la Mto Yordani! Yahwe ni jina lake! Shangilieni mbele zake!
Sing to God, make music to his name, his name is the Lord, praise him who rides on the clouds, and exult in his presence.
5 Baba wa yatima, na mwamuzi wa wajane, ni Mungu anayeishi mahali patakatifu.
Father of orphans, defender of widows, is God in his holy abode.
6 Mungu huwaweka wakiwa katika familia; yeye huwafungua wafungwa kwa kuimba bali waasi huishi katika ardhi kavu.
God brings home the lonely, he leads forth the prisoner to comfort, so that none but the rebel lives cheerless.
7 Mungu, wewe ulipoenda mbele ya watu wako, ulipotembea kupitia jangwani, (Selah)
God, when you went in front of your people in your march through the desert, (Selah)
8 nchi ilitetemeka; mbingu pia zilidondosha mvua katika uwepo wa Mungu, uweponi mwa Mungu wakati alipokuja Sinai, uweponi mwa Mungu, Mungu wa Israeli.
earth shook, the heavens poured rain at the presence of God, Sinai’s God at the presence of God, Israel’s God.
9 Wewe, Mungu, ulituma mvua nyingi; uliuimarisha urithi wako wakati ulipokuwa umechoka.
Rain in abundance, God, you did sprinkle, restoring the languishing land of your heritage.
10 Watu wako waliishi humo; Wewe, Mungu, uliutoa kwa wema wako kwa maskini.
A dwelling therein your people found: in your goodness, O God, you did care for the poor.
11 Bwana alitoa amri, na wale walio zitangaza walikuwa ni jeshi kuu.
The Lord spoke the glad tidings of victory, a great army of women proclaim it:
12 Wafalme wa majeshi wanakimbia, wanakimbia, na wanawake wakisubiri nyumbani kuvigawana wao na familia zao vilivyotekwa nyara.
“Kings of armies they flee, they flee, and the housewife divides the spoil:
13 Njiwa walio vikwa fedha wakiwa na mabawa ya njano ya dhahabu. Wakati baadhi ya watu wakikaa kati ya mifugo ya kondoo, kwa nini umefanya haya?
dove’s wings covered with silver and pinions with shimmer of gold,
14 Mwenyezi Mungu aliwatawanya Wafalme huko, ilikuwa kama vile wakati wa theluji juu ya Mlima Salmoni.
set with stones, like snow upon Zalmon.”
15 Mlima mkubwa ni milima wa mji wa Bashani; mlima mrefu ni mlima wa mji wa Bashani.
A mountain of God is the mountain of Bashan, a mountain of peaks is the mountain of Bashan.
16 Ewe mlima mrefu wa nchi, kwa nini unatazama kwa jicho la husuda, kwenye mlima ambao Mungu ameutaka kwa ajili ya mahali ambapo yeye ataishi? Hakika, Yahwe ataishi humo milele.
You high-peaked mountains, why look you askance at the mountain which God has desired for his home whereon the Lord will live forever?
17 Magari ya Mungu ni ishirini elfu, maelfu juu ya maelfu; Bwana yu kati yao katika mahari patakatifu, kama katika Sinai.
The chariots of God are twice ten thousand: the Lord came from Sinai, his holy place.
18 Wewe umepaa juu; uliwaongoza mateka; umepokea zawadi kutoka kati ya watu, hata kutoka kwa wale waliopigana dhidi yako, ili kwamba wewe, Yahwe Mungu, uweze kuishi huko.
You did mount the height with trains of your captives, and gifts that you had received from the people. The rebels shall live with the Lord God.
19 Abarikiwe Bwana, atubebeaye mizigo yetu, Mungu ambaye ni wokovu wetu. (Selah)
Blest be the Lord who sustains us daily, the God who is also our savior. (Selah)
20 Mungu wetu ni Mungu aokoaye; Yahwe Bwana ni yule awezaye kutuokoa sisi dhidi ya kifo.
Our God is a God who is savior. The ways of escape from death are known to the Lord God.
21 Lakini Bwana atapiga vichwa vya adui zake, mpaka kwenye ngozi ya kichwa yenye nywele ya wale watembeao katika makosa dhidi yake.
Yes, God will shatter the head of his foes the rough scalp of those who strut on in their sins.
22 Bwana alisema, “Nitawarudisha adui zangu kutoka Bashani; nitawarudisha kutoka katika kina cha bahari
The Lord said: “I will bring you home from Bashan, home from the depths of the sea,
23 ili kwamba upate kuwaangamiza adui zako, ukichovya mguu wako katika damu, na ili kwamba ndimi za mbwa wako zipate mlo wao kutoka kwa adui zenu.”
that your feet you may bathe in blood, and your dogs lick their share of the foe.”
24 Mungu, wameona maandamano yako, maandamano ya Mungu wangu, Mfalme wangu, kwenye mahali patakatifu.
In the temple appear God’s triumphal processions, processions in praise of my king and my God,
25 Waimbaji walitangulia, walifuatiwa na wapiga muziki, na katikati walikuwa wanawali wakicheza ngoma.
with singers in front, and minstrels behind, and maidens with timbrels between them, singing,
26 Mtukuzeni Mungu katika kusanyiko; msifuni Yahwe, ninyi ukoo wa kweli wa Israeli.
“You of the well-spring of Israel, bless the Lord God in the dance.”
27 Kuna Benjamini kwanza, kabila dogo, kisha viongozi wa Yuda na watu wao, viongozi wa Zabuloni na viongozi wa Naftali.
There, in front, is Benjamin the little, the princes of Judah beside them, the princes of Zebulon, princes of Naphtali.
28 Mungu wenu, Israeli, ameamuru nguvu zenu; uzifunue kwetu nguvu zako, Mungu, kama ulivyo zifunua wakati uliopita.
God, show your strength, your godlike might, as you did in the past,
29 Uzifunue nguvu zako kwetu toka katika hekalu la Yerusalemu, ambako wafalme huleta zawadi kwako.
from your temple that crowns Jerusalem. Kings shall bring tribute to you.
30 Pigeni kelele katika vita dhidi ya wanyama wa porini katika mianzi, dhidi ya watu, lile kundi la mafahari na ndama. Wafedhehesheni na kuwalazimisha wawaletee zawadi; watawanyeni watu wapendao kupigana vita.
Rebuke the beast of the reed, the herd of bulls, with the calves of the peoples. Trample down the lovers of lies. Scatter the nations whose joy is in war.
31 Wakuu watatoka katika Misri; Ethiopia itafanya haraka kuufikisha mkono wake kwa Mungu.
May they come from Egypt with gifts of oil, Ethiopia haste with full hands to God.
32 Mwimbieni Mungu, enyi falme za nchi; (Selah) mwimbieni sifa Yahwe.
Sing to God, O you kingdoms of earth, make melody to the Lord. (Selah)
33 Kwake yeye apitaye juu ya mbingu za mbingu, zilizokuwepo tangu zama za kale; tazama, yeye hupiga kelele kwa nguvu
Praise him who rides on the ancient heavens. See! He utters his voice, his mighty voice.
34 Tangazeni kuwa Mungu ni mwenye nguvu; enzi yake iko juu ya Israeli, na nguvu zake ziko angani.
Ascribe strength to the God over Israel, whose strength and majesty live in the skies.
35 Mungu, mahali pako patakatifu panatisha; Mungu wa Israeli, yeye huwapa watu wake nguvu na uweza. Atukuzwe Mungu.
Awe-inspiring is God in his holy place, it is Israel’s God who gives strength and might to his people. Blessed be God.

< Zaburi 68 >