< Zaburi 66 >

1 Mpigieni Mungu kelele za shangwe, nchi yote;
Al la ĥorestro. Kanto-psalmo. Ĝoje kriu al Dio tuta la tero.
2 Imbeni utukufu wa jina lake; mzitukuze sifa zake.
Muziku la gloron de Lia nomo, Faru honoron al Lia gloro.
3 Mwambieni Mugu, “Matendo yako yanatisha kama nini! Kwa ukuu wa nguvu zako maadui zako watajisalimisha kwako.
Diru al Dio: Kiel timindaj estas Viaj faroj! Pro Via granda forto kaŝiĝas antaŭ Vi Viaj malamikoj.
4 Nchi yote watakuabudu wewe na watakuimbia wewe; wataliimbia jina lako.” (Selah)
La tuta tero kliniĝas antaŭ Vi kaj kantas al Vi, Kantas Vian nomon. (Sela)
5 Njoni na mtazame kazi za Mungu; yeye anatisha katika matendo yake awatendeayo wanadamu.
Venu, kaj rigardu la farojn de Dio, Kiu estas timinda pro Siaj faroj inter la homidoj.
6 Aligeuza bahari kuwa nchi kavu; wao walitembea kwa mguu juu ya mto; huko tulishangilia katika yeye.
Li faris el maro sekan teron; Riveron oni transpaŝis piede; Tie ni ĝojis pro Li.
7 Yeye anatawala milele kwa nguvu zake; macho yake yanachunguza mataifa; waasi wasijivune. (Selah)
Li regas per Sia potenco eterne; Liaj okuloj rigardas la popolojn; La ribelantoj ne leviĝu. (Sela)
8 Mtukuzeni Mungu, enyi watu wa mataifa yote, sauti ya sifa zake isikike.
Laŭdu, ho popoloj, nian Dion, Kaj laŭte aŭdigu Lian gloron.
9 Yeye atuwekaye hai, naye hairuhusu miguu yetu iteleze.
Li donis vivon al nia animo, Kaj ne lasis falŝanceliĝi nian piedon.
10 Kwa maana wewe, Mungu, umetupima sisi, wewe umetupima kama inavyopimwa fedha.
Ĉar Vi esploris nin, ho Dio; Vi refandis nin, kiel oni refandas arĝenton.
11 Wewe ulituingiza sisi kwenye wavu; uliweka mzigo mzito viunoni mwetu.
Vi enirigis nin en kaptilon, Vi metis ŝarĝon sur niajn lumbojn;
12 Wewe uliwafanya watu wasafiri juu ya vichwa vyetu; tulipita motoni na majini, lakini ukatuleta mahali pa wazi palipo salama.
Vi rajdigis homojn sur niaj kapoj; Ni trapasis fajron kaj akvon, Sed Vi elirigis nin en bonstaton.
13 Nitaingia nyumbani mwako nikiwa na sadaka ya kuteketezwa; nitakulipa viapo vyangu
Mi eniros en Vian domon kun bruloferoj; Mi plenumos al Vi miajn promesojn,
14 ambavyo midomo yangu iliahidi na kinywa changu kiliongea nilipokuwa katika dhiki.
Kiujn eligis miaj lipoj kaj elparolis mia buŝo, Kiam mi estis en premo.
15 Nitakutolea sadaka ya kuteketezwa ya wanyama wanene pamoja na harufu nzuri ya kondoo waume; Nitatoa ng'ombe na mbuzi. (Selah)
Grasajn bruloferojn mi alportos al Vi kun fumo de virŝafoj; Mi oferos bovidojn kaj kaprojn. (Sela)
16 Njoni, msikie, ninyi nyote mnao mwabudu Mungu, nami nitatangaza yale yeye aliyoitendea roho yangu.
Venu, aŭskultu, ĉiuj, kiuj timas Dion; Kaj mi rakontos, kion Li faris por mia animo.
17 Nilimlilia kwa kinywa changu, naye alipendezwa na ulimi wangu.
Al Li mi vokis per mia buŝo, Kaj Lia glorado estis sub mia lango.
18 Kama ningelikuwa na dhambi ndani ya moyo wangu, Bwana asingenisikiliza.
Se mi vidus maljustaĵon en mia koro, Mia Sinjoro min ne aŭskultus;
19 Lakini Mungu hakika amesikia; amesikia sautiya kuomba kwangu.
Sed Dio aŭskultis, Li atentis la voĉon de mia preĝo.
20 Atukuzwe Mungu, ambaye hakuyakataa maombi yangu wala kuweka uaminifu wa agano lake mbali nami.
Glorata estu Dio, Kiu ne forpuŝis mian preĝon kaj ne rifuzis al mi Sian bonecon.

< Zaburi 66 >