< Zaburi 64 >

1 Sikia sauti yangu, Mungu, usikilize malalamiko yangu; unilinde dhidi ya hofu ya adui zangu.
Escucha, oh ʼElohim, la voz de mi queja: Preserva mi vida del terror de perversos.
2 Unifiche dhidi ya mipango ya siri ya wafanyao maovu, unifiche dhidi ya watendao vurugu ya udhalimu.
Ocúltame de la conspiración de malhechores, Del tumulto de los que hacen iniquidad,
3 Wao wamenoa ndimi zao kama panga; wamelenga mishale yao, maneno machungu,
Que afilan sus lenguas como una espada, Y la emplean como su flecha en un lenguaje amargo
4 ili kwamba waweze kupiga kutoka mahali pa siri kwenda kwa mtu asiye na hatia; wampige yeye kwa ghafla nao wasihofu lolote.
Para dispararlas en oculto al inocente. De repente disparan sus flechas, sin que teman.
5 Wao wanahamasishana wenyewe katika kupanga uovu; wanashauriana pamoja wao binafsi ili kuweka mitego; nao husema, “Ni nani atakayetuona?”
Se animan unos a otros en su perverso designio Y planean esconder trampas. Dicen: ¿Quién las verá?
6 Wanabuni mipango ya dhambi; “Tumemaliza,” wanasema, “ni mpango makini.” Mawazo ya ndani na mioyo ya watu ni ya kina.
Traman injusticias y dicen: Estamos listos con una conspiración bien concebida. Tanto el pensamiento íntimo como el corazón del hombre son profundos.
7 Lakini Mungu atawapiga wao; ghafla watajeruhiwa kwa mishale yake.
Pero ʼElohim les dispara una flecha. De repente vendrán sus plagas.
8 Watafanywa kuwa mashakani, kwa kuwa ndimi zao wenyewe ziko kinyume nao; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao.
Así que ellas los hacen tropezar. Los que los ven menean la cabeza.
9 Watu wote wataogopa na kutangaza matendo ya Mungu. Kwa hekima watafikiria kuhusu kile yeye ametenda.
Entonces temerán todos los hombres. Proclamarán la obra de ʼElohim Y entenderán sus hechos.
10 Wenye haki watakuwa na furaha kuhusu Yahwe nao watakimbilia kwake; wote wenye haki moyoni watajivuna katika yeye.
El justo se alegrará en Yavé, Y se confiará en Él. Se gloriarán todos los rectos de corazón.

< Zaburi 64 >