< Zaburi 64 >

1 Sikia sauti yangu, Mungu, usikilize malalamiko yangu; unilinde dhidi ya hofu ya adui zangu.
In finem, Psalmus David. Exaudi Deus orationem meam cum deprecor: a timore inimici eripe animam meam.
2 Unifiche dhidi ya mipango ya siri ya wafanyao maovu, unifiche dhidi ya watendao vurugu ya udhalimu.
Protexisti me a conventu malignantium: a multitudine operantium iniquitatem.
3 Wao wamenoa ndimi zao kama panga; wamelenga mishale yao, maneno machungu,
Quia exacuerunt ut gladium linguas suas: intenderunt arcum rem amaram,
4 ili kwamba waweze kupiga kutoka mahali pa siri kwenda kwa mtu asiye na hatia; wampige yeye kwa ghafla nao wasihofu lolote.
ut sagittent in occultis immaculatum.
5 Wao wanahamasishana wenyewe katika kupanga uovu; wanashauriana pamoja wao binafsi ili kuweka mitego; nao husema, “Ni nani atakayetuona?”
Subito sagittabunt eum, et non timebunt: firmaverunt sibi sermonem nequam. Narraverunt ut absconderent laqueos: dixerunt: Quis videbit eos?
6 Wanabuni mipango ya dhambi; “Tumemaliza,” wanasema, “ni mpango makini.” Mawazo ya ndani na mioyo ya watu ni ya kina.
Scrutati sunt iniquitates: defecerunt scrutantes scrutinio. Accedet homo ad cor altum:
7 Lakini Mungu atawapiga wao; ghafla watajeruhiwa kwa mishale yake.
et exaltabitur Deus. Sagittæ parvulorum factæ sunt plagæ eorum:
8 Watafanywa kuwa mashakani, kwa kuwa ndimi zao wenyewe ziko kinyume nao; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao.
et infirmatæ sunt contra eos linguæ eorum. Conturbati sunt omnes qui videbant eos:
9 Watu wote wataogopa na kutangaza matendo ya Mungu. Kwa hekima watafikiria kuhusu kile yeye ametenda.
et timuit omnis homo. Et annunciaverunt opera Dei: et facta eius intellexerunt.
10 Wenye haki watakuwa na furaha kuhusu Yahwe nao watakimbilia kwake; wote wenye haki moyoni watajivuna katika yeye.
Lætabitur iustus in Domino, et sperabit in eo, et laudabuntur omnes recti corde.

< Zaburi 64 >