< Zaburi 63 >

1 Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
Ó Deus, tu és o meu Deus, de madrugada te buscarei: a minha alma tem sede de ti; a minha carne te deseja muito em uma terra seca e cançada, onde não há água
2 Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
Para ver a tua fortaleza e a tua glória, como te vi no santuário.
3 Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
Porque a tua benignidade é melhor do que a vida; os meus lábios te louvarão.
4 Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
Assim eu te bendirei enquanto viver: em teu nome levantarei as minhas mãos.
5 Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
A minha alma se fartará, como de tutano e de gordura; e a minha boca te louvará com alegres lábios,
6 nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
Quando me lembrar de ti na minha cama, e meditar em ti nas vigílias da noite.
7 Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
Porque tu tens sido o meu auxílio; portanto na sombra das tuas asas me regozijarei.
8 Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
A minha alma te segue de perto: a tua dextra me sustenta.
9 Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
Mas aqueles que procuram a minha alma para a destruir, irão para as profundezas da terra.
10 watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
Cairão à espada, serão uma ração para as raposas.
11 Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.
Mas o rei se regozijará em Deus; qualquer que por ele jurar se glóriará; porque se taparão as bocas dos que falam a mentira.

< Zaburi 63 >