< Zaburi 63 >

1 Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
Ein Psalm Davids, als er in der Wüste Judah war. Gott, mein Gott bist Du, nach Dir suche ich frühe, nach Dir dürstet meine Seele, nach Dir schmachtet mein Fleisch im Lande der Dürre, und wenn matt, ohne Wasser.
2 Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
So habe ich nach dir im Heiligtum geschaut, um Deine Stärke und Herrlichkeit zu sehen.
3 Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
Denn besser als Leben ist Deine Barmherzigkeit. Meine Lippen sollen Dich preisen.
4 Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
So will ich segnen Dich in meinem Leben, will in Deinem Namen meine Hände erheben.
5 Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
Gleich wie an Fett und an Feistem sich sättigt meine Seele, und mit Lippen der Lobpreisung lobt Dich mein Mund,
6 nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
Wenn Deiner ich gedenke auf meiner Lagerstätte, in Nachtwachen sinne über Dich,
7 Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
Daß Du mir Beistand warst, darum lobpreise ich im Schatten Deiner Flügel.
8 Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
An Dir hängt meine Seele, mich erhält Deine Rechte.
9 Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
Sie aber, die nach meiner Seele trachten, sie zu zerstören: Laß sie kommen in der Erde Unterstes.
10 watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
Lasse sie durch die Hand des Schwertes vergehen, Schakalen zum Anteil werden.
11 Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.
Der König aber wird fröhlich sein in Gott, und jeder sich rühmen, der bei Ihm schwört, wenn der Mund wird verstopft denen, so Lüge reden.

< Zaburi 63 >