< Zaburi 63 >

1 Mungu, wewe ni Mungu wangu! Ninakutafuta wewe kwa bidii, moyo wangu unakiu yako, mwili wangu unakutamani sana wewe, katika ukame na nchi iliyochoka mahali ambapo hakuna maji.
A psalm of David when was he in [the] wilderness of Judah. O God - [are] God my you I am seeking earnestly you it is thirsty for you - self my it longs for you flesh my in a land dry and weary not water.
2 Hivyo nimekutafuta wewe katika watu watakatifu kuona nguvu zako na utukufu wako.
Thus in the sanctuary I have seen you to see strength your and glory your.
3 Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakusifu wewe.
For [is] good covenant loyalty your more than life lips my they will extol you.
4 Hivyo nitakutukuza wewe niwapo hai; kwa jina lako nitainua mikono yangu juu.
Thus I will bless you in life my in name your I will lift up hands my.
5 Itakuwa kana kwamba nilikula mlo wa mafuta na wenye kunona, kwa midomo ya furaha kinywa changu kitakusifu wewe,
Like fat and fatness it will be satisfied self my and lips of cries of joy it will praise [you] mouth my.
6 nikufikiripo kitandani mwangu na kukutafakari wewe wakati wa saa za usiku.
If I have remembered you on beds my in [the] night-watches I meditate on you.
7 Kwa maana umekuwa msaada wangu, na katika uvuli wa mbawa zako ninafurahia.
For you are a help of me and in [the] shadow of wings your I shout for joy.
8 Ninashikamana nawe; mkono wako wa kuume unanisaidia.
It clings self my after you me it supports right [hand] your.
9 Lakini wale watafutao kuuharibu uhai wangu wataenda chini kwenye sehemu ya chini kabisa ya nchi;
And they to destruction they are seeking life my they will go in [the] lower parts of the earth.
10 watakabidhiwa kwa wale ambao mikono yao hutumia upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
People will pour him over [the] hands of [the] sword [the] portion of foxes they will be.
11 Bali mfalme atashangilia katika Mungu; yeyote anaye apa kupitia yeye atajivunia yeye, lakini vinywa ya wale wasemao uongo watanyamazishwa.
And the king he will rejoice in God he will boast every [one who] swears an oath by him for it will be shut up [the] mouth of [those who] speak falsehood.

< Zaburi 63 >