< Zaburi 62 >

1 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; wokovu wangu watoka kwake.
For the leader. On jeduthun. A psalm of David. I wait alone in silence for God; From him comes my help.
2 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa kamwe.
Yes, he is my rock, my help, my retreat, I shall not be shaken too sorely.
3 Mpaka lini, ninyi nyote, mtamshambulia mtu, ili kwamba mumpindue yeye kama ukuta ulio inama au kama fensi isiyo imara?
How long will you, all of you, batter a man, as one might a leaning wall?
4 Wanashauliana naye ili tu kumshusha chini kutoka kwenye nafasi yake heshimiwa; wao wanapenda kuongea uongo; wanambariki yeye kwa midomo yao, lakini mioyoni mwao wana mlaani yeye. (Selah)
From his height they are planning to topple him. They take pleasure in falsehood; they bless with their mouth, but inwardly they curse. (Selah)
5 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; kwa maana matumaini yangu yako kwake.
I wait alone in silence for God; for from him comes my hope.
6 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa.
Yes, he is my rock, my help, my retreat, I shall not be shaken too sorely.
7 Na Mungu ni wokovu wangu na utukufu wangu; mwamba wa nguvu yangu na kimbilio langu salama liko katika Mungu.
On God rests my honor and safety, in God is my strong rock, my refuge.
8 Mwaminini Mungu wakati wote, ninyi watu; mimina moyo wako mbele zake; Mungu ni kimbilio salama kwa ajili yetu. (Selah)
Trust in him, all you people assembled, pour out your heart in his presence; God is a refuge for us. (Selah)
9 Hakika watu wenye msimamo mdogo ni ubatili, na watu wenye msimamo mkubwa ni waongo; wao watakuwa wepesi kwenye mzani; uzito wao pamoja ni wepesi kuliko kitu chochote.
The lowly are nought but a breath, the lofty are but an illusion: in the balances up they go, they are lighter than breath altogether.
10 Usiamini katika ukandamizaji au wizi; usitumainie utajiri, maana hawatazaa matunda; usiuweke moyo wako kwenye hivyo.
Trust not in gain of extortion, set no vain hopes in robbery. As for wealth, if it bears fruit, set not your heart upon it.
11 Mungu ameongea mara moja, mara mbili nimesikia hili: nguvu ni za Mungu.
One thing God has uttered, two things there are which I heard that power belongs to God,
12 Pia kwako, Bwana, ni uaminifu wa agano, maana humlipa kila mtu kwa kile alichokifanya.
and to you, too, O Lord, belongs kindness; for you requite each person according to what they have done.

< Zaburi 62 >