< Zaburi 56 >

1 Uwe na huruma nami, Mungu, kwa maana watu wananishambulia! Muda wote wale wanao pigana nami hunikaribia zaidi ili wanishambulie.
For the leader. On jonath elem rehokim. Of David. A michtam, when the Philistines seized him in Gath. O God, be gracious to me, for people trample upon me, all the day righting and pressing me.
2 Adui zangu hunikanyaga muda wote; maana ni wengi ambao kwa kiburi hupigana dhidi yangu.
All the day enemies trample me; many there be who contend with me bitterly.
3 Wakati nina woga, nitaweka imani yangu katika wewe.
In the day of my terror I trust in you.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu - nimeweka imani yangu katika Mungu; sitaogopa; mtu wa kawaida atanifanya nini?
In God I maintain my cause, in God I fearlessly trust. What can flesh do to me?
5 Muda wote wanayageuza maneno yangu; mawazo yao yote yako kinyume na mimi kwa ajili ya uovu.
They torture me all the day, they ceaselessly plan to hurt me,
6 Wanajikusanya kwa pamoja, wanajificha wenyewe, na kuzifuatilia hatua zangu, wakisubiri kuniua.
banded together in secret, watching my every step, as those who hope for my death.
7 Usiwaache waikimbie adhabu yako kwa ajili ya uovu wao. Uwaangushe watu chini katika hasira yako, Mungu.
Pay them out for their sin, O God, hurl down the strong in your anger.
8 Wewe unahesabu kutangatanga kwangu na kuweka machozi yangu kwenye chupa yako; je, hayako kitabuni mwako?
You yourself count my wanderings. Put in your bottle my tears are they not in your book?
9 Ndipo maadui zangu watakimbia katika siku ile nikuitapo wewe; hili najua, kwamba Mungu yupo kwa ajili yangu.
Then shall my foes be turned back in the day that I call. Of this I am sure, because God is for me.
10 Katika Mungu ambaye neno lake ninalisifu, katika Yahwe ambaye neno lake ninalisifu,
In God I maintain my cause, in the Lord I maintain my cause.
11 katika Mungu ninaamini, sitaogopa. Yeyote atanifanya nini?
In God I fearlessly trust, what can people do to me?
12 Wajibu wa kutimiza viapo vyangu kwako uko juu yangu, Mungu; nitatoa sadaka ya shukurani.
Your vows are upon me, O God, I will render thank-offerings to you;
13 Kwa kuwa umeokoa uhai wangu na mauti; umezuia miguu yangu isianguke, ili kwamba niweze kutembea mbele ya Mungu katika nuru ya uhai.
because you have saved me from death, my feet from stumbling, to the end that I walk before God in the light of the living.

< Zaburi 56 >