< Zaburi 56 >

1 Uwe na huruma nami, Mungu, kwa maana watu wananishambulia! Muda wote wale wanao pigana nami hunikaribia zaidi ili wanishambulie.
TO THE OVERSEER. [SET] ON “A SILENT DOVE FAR OFF.” A MIKTAM OF DAVID, IN THE PHILISTINES’ TAKING HOLD OF HIM IN GATH. Favor me, O God, for man swallowed me up, All the day fighting he oppresses me,
2 Adui zangu hunikanyaga muda wote; maana ni wengi ambao kwa kiburi hupigana dhidi yangu.
My enemies have swallowed up all the day, For many [are] fighting against me, O Most High,
3 Wakati nina woga, nitaweka imani yangu katika wewe.
[In] the day I am afraid I am confident toward You.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu - nimeweka imani yangu katika Mungu; sitaogopa; mtu wa kawaida atanifanya nini?
In God I praise His word, in God I have trusted, I do not fear what flesh does to me.
5 Muda wote wanayageuza maneno yangu; mawazo yao yote yako kinyume na mimi kwa ajili ya uovu.
All the day they wrest my words, All their thoughts [are] for evil concerning me,
6 Wanajikusanya kwa pamoja, wanajificha wenyewe, na kuzifuatilia hatua zangu, wakisubiri kuniua.
They assemble, they hide, they watch my heels, When they have expected my soul.
7 Usiwaache waikimbie adhabu yako kwa ajili ya uovu wao. Uwaangushe watu chini katika hasira yako, Mungu.
They escape by iniquity, In anger put down the peoples, O God.
8 Wewe unahesabu kutangatanga kwangu na kuweka machozi yangu kwenye chupa yako; je, hayako kitabuni mwako?
You have counted my wandering, You place my tear in Your bottle, Are they not in Your scroll?
9 Ndipo maadui zangu watakimbia katika siku ile nikuitapo wewe; hili najua, kwamba Mungu yupo kwa ajili yangu.
Then turn back my enemies in the day I call. This I have known, that God [is] for me.
10 Katika Mungu ambaye neno lake ninalisifu, katika Yahwe ambaye neno lake ninalisifu,
In God I praise the word, In YHWH I praise the word.
11 katika Mungu ninaamini, sitaogopa. Yeyote atanifanya nini?
In God I trusted, I do not fear what man does to me,
12 Wajibu wa kutimiza viapo vyangu kwako uko juu yangu, Mungu; nitatoa sadaka ya shukurani.
On me, O God, [are] Your vows, I repay thank-offerings to You.
13 Kwa kuwa umeokoa uhai wangu na mauti; umezuia miguu yangu isianguke, ili kwamba niweze kutembea mbele ya Mungu katika nuru ya uhai.
For You have delivered my soul from death, Do You not [keep] my feet from falling? To habitually walk before God in the light of the living!

< Zaburi 56 >