< Zaburi 52 >

1 Kwa nini wewe unajivunia kufanya uovu, wewe mtu mwenye nguvu? Uaminifu wa agano la Mungu huja kila siku.
For the leader. A maskil of David, when Doeg the Edomite came and told Saul that David had gone to Abimelech’s house. Why glory in mischief, you hero? God’s kindness is all the day.
2 Ulimi wako hupanga uharibifu kama wembe mkali, na kufanya udanganyifu.
Engulfing ruin you plot, your tongue like a razor sharpened, you practiser of deceit.
3 Wewe unapenda uovu kuliko wema na udanganifu kuliko kuongea haki. (Selah)
Evil, not good, you love, and falsehood, not words of truth. (Selah)
4 Wewe hupenda maneno ambayo huwaumiza wengine, wewe ulimi mdanganyifu.
But you love all words that devour, and a tongue that is given to deceit.
5 Vivyo hivyo Mungu atakuadhibu wewe milele; yeye atakuchukua na kukuondoa katika hema yako na kukung'oa katika ardhi ya uhai. (Selah)
But God, on his part, shall destroy you forever, grasp you and pluck you out of your tent, and root you out of the land of the living. (Selah)
6 Wenye haki pia wataona na kuogopa; watamcheka na kusema,
Smitten with awe at the sight, the righteous shall laugh at you.
7 “Tazama, huyu ni mtu ambaye hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake la usalama, bali aliamini katika wingi wa mali zake, naye alikuwa na nguvu alipowaharibu wengine.”
“Look” (they will say) “at the hero who did not make God his stronghold, but trusted in his great wealth and in the strength of his riches.”
8 Lakini kwangu mimi, niko kama mti bora wa mzeituni katika nyumba ya Mungu; Nami nitaamini uaminifu wa agano la Mungu milele na milele.
But I am like a fresh olive-tree in the house of God. I trust in the kindness of God for ever and evermore.
9 Nitakushukuru wewe daima kwa uliyo tenda. Nitalisubiri jina lako, kwa sababu ni zuri, uweponi mwa wantu wako wa kimungu.
I will render you thanks for ever for what you have done. I will tell how good you are in the presence of those who love you.

< Zaburi 52 >