< Zaburi 52 >

1 Kwa nini wewe unajivunia kufanya uovu, wewe mtu mwenye nguvu? Uaminifu wa agano la Mungu huja kila siku.
[For the Chief Musician. A contemplation by David, when Doeg the Edomite came and told Saul, "David has come to Abimelech's house."] Why do you boast of mischief, mighty man? God's loving kindness endures continually.
2 Ulimi wako hupanga uharibifu kama wembe mkali, na kufanya udanganyifu.
Your tongue plots destruction, like a sharp razor, working deceitfully.
3 Wewe unapenda uovu kuliko wema na udanganifu kuliko kuongea haki. (Selah)
You love evil more than good, lying rather than speaking the truth. (Selah)
4 Wewe hupenda maneno ambayo huwaumiza wengine, wewe ulimi mdanganyifu.
You love all devouring words, you deceitful tongue.
5 Vivyo hivyo Mungu atakuadhibu wewe milele; yeye atakuchukua na kukuondoa katika hema yako na kukung'oa katika ardhi ya uhai. (Selah)
God will likewise destroy you forever. He will take you up, and pluck you out of your tent, and root you out of the land of the living. (Selah)
6 Wenye haki pia wataona na kuogopa; watamcheka na kusema,
The righteous also will see it, and fear, and laugh at him, saying,
7 “Tazama, huyu ni mtu ambaye hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake la usalama, bali aliamini katika wingi wa mali zake, naye alikuwa na nguvu alipowaharibu wengine.”
"Look, this is the man who did not make God his strength, but trusted in the abundance of his riches, and was confident in his desire."
8 Lakini kwangu mimi, niko kama mti bora wa mzeituni katika nyumba ya Mungu; Nami nitaamini uaminifu wa agano la Mungu milele na milele.
But as for me, I am like a green olive tree in God's house. I trust in God's loving kindness forever and ever.
9 Nitakushukuru wewe daima kwa uliyo tenda. Nitalisubiri jina lako, kwa sababu ni zuri, uweponi mwa wantu wako wa kimungu.
I will give you thanks forever, because you have done it. I will hope in your name, for it is good, in the presence of your faithful ones.

< Zaburi 52 >