< Zaburi 50 >

1 Mungu, Mwenye nguvu, Yahwe, amenena naye aliita nchi toka mawio ya jua mpaka machweo yake.
[A Psalm by Asaph.] The Mighty One, God, Jehovah, speaks, and summons the earth from the rising of the sun to its setting.
2 Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
Out of Zion, the perfection of beauty, God shines forth.
3 Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
Our God comes, and does not keep silent. A fire devours before him. It is very stormy around him.
4 Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
He calls to the heavens above, to the earth, that he may judge his people:
5 Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
"Gather my faithful ones together to me, those who have made a covenant with me by sacrifice."
6 Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
The heavens shall declare his righteousness, for God himself is judge. (Selah)
7 Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
"Hear, my people, and I will speak; Israel, and I will testify against you. I am God, your God.
8 Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
I do not rebuke you for your sacrifices. Your burnt offerings are continually before me.
9 Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
I have no need for a bull from your stall, nor male goats from your pens.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
For every animal of the forest is mine, and the livestock on a thousand hills.
11 Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
I know all the birds of the mountains. The wild animals of the field are mine.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
If I were hungry, I would not tell you, for the world is mine, and all that is in it.
13 Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
Will I eat the flesh of bulls, or drink the blood of goats?
14 Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
Offer to God the sacrifice of thanksgiving. Pay your vows to the Most High.
15 Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa
Call on me in the day of trouble. I will deliver you, and you will honor me."
16 Lakini kwa waovu Mungu anasema, “Inawahusu nini kuitangaza hali yangu, kwamba ninyi mmeliweka agano langu mdomoni mwenu,
But to the wicked God says, "What right do you have to declare my statutes, that you have taken my covenant on your lips,
17 wakati ninyi mnayachukia maelekezo na mnayatupa maneno yangu?
seeing you hate instruction, and throw my words behind you?
18 Mumuanapo mwizi, ninyi hukubaliana naye; ninyi na mnashirikiana na wale wafanyao uasherati.
When you saw a thief, you consented with him, and have participated with adulterers.
19 Mwautoa mdomo wenu kwa mabaya, huelezea udanganyifu.
"You give your mouth to evil. Your tongue frames deceit.
20 Mnakaa na kuongea dhidi ya ndugu yenu; na kukashfu mwana wa mama yenu.
You sit and speak against your brother. You slander your own mother's son.
21 Mmefanya mambo haya, lakini nimekaa kimya, hivyo mlidhani kuwa ni mtu flani nilliye kama ninyi mlivyo. Lakini nitawakaripia ninyi na kuwafunua, mbele ya macho yenu, mambo yote miliyofanya.
You have done these things, and I kept silent. You thought that I was just like you. I will rebuke you, and accuse you in front of your eyes.
22 Mlitilie maanani hili, ninyi mnao msahau Mungu, vinginevyo nitawakata ninyi vipande vipande, na hatakuwepo yeyote wakuja kuwasaidia!
"Now consider this, you who forget God, lest I tear you into pieces, and there be none to deliver.
23 Yule atoaye sadaka ya shukurani hunitukuza, na yeyote apangaye njia zake katika namna iliyo sahihi nitamuonesha wokovu wa Mungu.”
Whoever offers the sacrifice of thanksgiving glorifies me; and to him who orders his conduct I will show the salvation of God."

< Zaburi 50 >