< Zaburi 48 >

1 Yahwe ndiye aliye mkuu na mwenyekusifiwa sana, katika mji wa Mungu wetu kwenye mlima wake mtakatifu.
Great is Adonai, and greatly to be praised, in the city of our God, in his holy mountain.
2 Ni mzuri katika mwinuko wake, furaha ya nchi yote, ni mlima Sayuni, kwenye upande wa kaskazini, mji wa Mfalme mkuu.
Beautiful in elevation, the joy of the whole earth, is Mount Zion [Mountain ridge, Marking], on the north sides, the city of the great King.
3 Mungu amejifunua mwenyewe katika jumba lake la kifahari kama kimbilio la usalama.
In its citadels God has revealed himself as a strong defense.
4 Maana, tazama, wafalme walikusanyika wenyewe; wote pamoja walipita.
For, behold, the kings assembled themselves, they passed by together.
5 Nao waliuona, wakashangaa; walifadhaika, na wakaharakisha kuondoka.
They saw it, then they were amazed. They were dismayed. They hurried away.
6 Pale pale tetemeko liliwashikilia, maumivu makali kama mwanamke anaye zaa.
Trembling took hold of them there, pain, as of a woman in travail.
7 Kwa upepo wa mashariki wewe huivunja meli ya Tarshishi.
With the east wind, you break the ships of Tarshish.
8 Kama tulivyo sikia, vivyo hivyo tumeona katika mji wa Yahwe wa majeshi, katika mji wa Mungu wetu; Mungu atautunza milele. (Selah)
As we have sh'ma ·heard obeyed·, so we have seen, in the city of Adonai Tzva'ot [Yahweh Commander of heaven’s armies], in the city of our God. God will establish it forever. (Selah) ·contemplation with musical interlude·.
9 Tumeutafakari uaminifu wa agano lako, Mungu, katikati ya hekalu lako.
We have thought about your cheshed ·loving-kindness·, God, in the middle of your temple.
10 Kama lilivyo jina lako, Mungu, hivyo ndivyo zilivyo sifa zako mpaka miisho ya dunia; mkono wako wa kuume umejaa haki.
As is your name, God, so is your tehilah ·praise song· to the ends of the earth. Your right hand is full of righteousness.
11 Milma Sayuni na ufurahi, nao wana wa Yuda washangilie kwa sababu ya amri ya haki yako.
Let Mount Zion [Mountain ridge, Marking] be glad! Let the daughters of Judah [Praised] rejoice, Because of your judgments.
12 Tembeeni katika Mlima Sayuni, muuzungukie mji,
Walk about Zion [Mountain ridge, Marking], and go around her. Number its towers.
13 mzitazame kwa makini nguzo zake, na mtazame majumba yake ya kifahari ili kwamba muweze kuwasimulia kizazi kijacho.
Mark well her bulwarks. Consider her palaces, that you may tell it to the next generation.
14 Kwa kuwa huyu Mungu ni Mungu wetu milele na milele; naye atakuwa kiongozi wetu mpaka kufa.
For this God is our God forever and ever. He will be our guide even to death.

< Zaburi 48 >