< Zaburi 47 >

1 Pigeni makofi, enyi watu wote; mpigieni Mungu kelele za ushindi.
For the leader. Of the Korahites. A psalm. Clap your hands, all you peoples: shout to God in ringing cries.
2 Kwa maana Yahwe Aliye Juu anatisha; ni Mfalme mkuu dunia yote.
For the Lord is most high and dread, a great king over all the earth.
3 Yeye anawatiisha chini yetu na mataifa chini ya miguu yetu.
He subdues the peoples under us, the nations under our feet;
4 Yeye huchagua urithi kwa ajili yetu, utukufu wa Yakobo ambaye alimpenda. Serah
he chooses our heritage for us, the glory of Jacob whom he loves. (Selah)
5 Mungu ameinuliwa juu kwa shangwe, Kwa mbiu ya shangwe Yahwe yu juu.
God is gone up with a shout, the Lord with the sound of a trumpet.
6 Mwimbieni Mungu sifa, imbeni sifa; mwimbieni sifa Mfalme wetu, imbeni sifa.
Sing praise to our God, sing praises: sing praise to our king, sing praises.
7 Kwa maana Mungu ni Mfalme duniani kote; mwimbieni mkiwa na uelewa.
For king of all earth is he: praise God in a skilful song.
8 Mungu anatawala mataifa yote; Mungu hukaa kwenye kiti cha enzi.
God is king over all the nations, God sits on his holy throne.
9 Wakuu wa watu wamekusanyika pamoja kwa watu wa Mungu wa Ibrahimu; kwa kuwa ngao za duniani ni za Mungu; yeye ameinuliwa juu sana.
Princes of nations gather with the people of Abraham’s God: for the shields of the earth are God’s; greatly exalted is he.

< Zaburi 47 >