< Zaburi 46 >

1 Mungu kwetu ni kimbilio la usalama na nguvu, upatikanao tele wakati wa mateso.
[For the Chief Musician. By the sons of Korah. According to Alamoth.] God is our refuge and strength, a very present help in trouble.
2 Hivyo hatutaogopa, hata kama dunia italazimika kubadilika, hata kama milima italazimika kutetemeka na kuangukia kwenye mtima wa bahari, hata kama maji yatavuma kwa kishindo kikuu,
Therefore we won't be afraid, though the earth changes, though the mountains are shaken into the heart of the seas;
3 hata kama milima itatetemeka kwa vurugu ya maji. (Selah)
though its waters roar and are troubled, though the mountains tremble with their swelling. (Selah)
4 Kuna mto, mikondo yake huufanya mji wa Mungu kufurahi, mahali patakatifu pa hema ya Aliye Juu.
There is a river, the streams of which make the city of God glad, the holy place of the tents of the Most High.
5 Mungu yuko katikati yake; naye hatasogezwa; Mungu atamsaidia, naye atafanya hivyo asubuhi na mapema.
God is in her midst. She shall not be moved. God will help her at dawn.
6 Mataifa yalikasirika na falme zikataharuki; yeye alipaza sauti yake, na nchi ikayeyuka.
The nations raged. The kingdoms were moved. He lifted his voice, and the earth melted.
7 Yahwe wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. (Selah)
Jehovah of hosts is with us. The God of Jacob is our refuge. (Selah)
8 Njoni, mtazame matendo ya Yahwe, uharibifu alioufanya juu ya nchi.
Come, see Jehovah's works, what desolations he has made in the earth.
9 Anaisitisha vita kwenye nchi; yeye anauvunja upinde na kuikata vipande vipande mishale; anazichoma ngao.
He makes wars cease throughout the earth. He breaks the bow, and shatters the spear. He burns the chariots in the fire.
10 Mkae kimya na mjue kuwa mimi ni Mungu; nitainuliwa juu ya nchi.
"Be still, and know that I am God. I will be exalted among the nations. I will be exalted in the earth."
11 Mungu wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. Serah
Jehovah of hosts is with us. The God of Jacob is our refuge. (Selah)

< Zaburi 46 >