< Zaburi 44 >

1 Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
We have sh'ma ·heard obeyed· with our ears, God; our fathers have told us, what work you did in their days, in the days of old.
2 Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
You drove out the nations with your hand, but you planted them. You afflicted the peoples, but you spread them abroad.
3 Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
For they didn’t get the land in possession by their own sword, neither did their own arm save them; but your right hand, and your arm, and the light of your face, because you were favorable to them.
4 Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
You are my King, God. Enjoin yishu'ah ·deliverance· for Jacob [Supplanter]!
5 Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
Through you, will we push down our adversaries. Through your name, will we tread them under who rise up against us.
6 Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
For I will not trust in my bow, neither shall my sword save me.
7 Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
But you have saved us from our adversaries, and have shamed those who hate us.
8 Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
In God we have made our boast all day long, we will yadah ·extend hands in thankful praise· to your name forever. (Selah) ·contemplation with musical interlude·.
9 Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
But now you rejected us, and brought us to dishonor, and don’t go out with our armies.
10 Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
You make us turn back from the adversary. Those who hate us take plunder for themselves.
11 Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
You have made us like sheep for food, and have scattered us among the nations.
12 Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
You sell your people for nothing, and have gained nothing from their sale.
13 Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
You make us a reproach to our neighbors, a scoffing and a derision to those who are around us.
14 Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
You make us a byword among the nations, a shaking of the head among the peoples.
15 Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
All day long my dishonor is before me, and shame covers my face,
16 kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
At the taunt of one who reproaches and verbally abuses, because of the enemy and the avenger.
17 Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
All this has come on us, yet have we not forgotten you, Neither have we been false to your covenant ·binding contract between two or more parties·.
18 Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
Our heart has not turned back, neither have our steps strayed from your path,
19 Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
Though you have crushed us in the haunt of jackals, and covered us with the shadow of death.
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
If we have forgotten the name of our God, or spread out our hands to a strange deity;
21 Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
won’t God search this out? For he knows the secrets of the heart.
22 Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
Yes, for your sake we are killed all day long. We are regarded as sheep for the slaughter.
23 Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
Wake up! Why do you sleep, Lord? Arise! Don’t reject us forever.
24 Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
Why do you hide your face, and forget our affliction and our oppression?
25 Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
For our soul is bowed down to the dust. Our body clings to the earth.
26 Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.
Rise up to help us. Redeem us for your cheshed ·loving-kindness’· sake.

< Zaburi 44 >