< Zaburi 44 >

1 Mungu, tumesikia kwa masikio yetu, baba zetu wametuambia kazi uliyofanya katika siku zao, siku za kale.
For the end, a Psalm for instruction, for the sons of Core. O God, we have heard with our ears, our fathers have told us, the work which you wrought in their days, in the days of old.
2 Uliwafukuza mataifa kwa mkono wako, lakini ukawafanya watu wetu kuishi humo; wewe uliwataabisha mataifa, lakini ukawaeneza watu wetu katika nchi.
Your hand utterly destroyed the heathen, and you did plant them: you did afflict the nations, and cast them out.
3 Kwa maana hawakupata umiliki wa nchi kwa upanga wao, wala mkono wao wenyewe haukuwaokoa; bali mkono wako wakuume, mkono wako, na nuru ya uso wako, na kwa sababu uliwaridhia.
For they inherited not the land by their [own] sword, and their [own] arm did not deliver them; but your right hand, and your arm, and the light of your countenance, because you were well pleased in them.
4 Mungu, wewe ni Mfalme wangu, amuru ushindi kwa ajili ya Yakobo.
You are indeed my King and my God, who command deliverances for Jacob.
5 Kwa uweza wako tutawaangusha chini maadui zetu; kwa jina lako tutatembea juu yao, wale wanao inuka dhidi yetu.
In you will we push down our enemies, and in your name will we bring to nothing them that rise up against us.
6 Kwa maana sitauamini upinde wangu, wala upanga wangu hautaniokoa.
For I will not trust in my bow, and my sword shall not save me.
7 Bali wewe ndeye uliyetuokoa na adui zetu, na umewaaibisha wale watuchukiao.
For you have saved us from them that afflicted us, and have put to shame them that hated us.
8 Katika Mungu tumefanywa kujivuna siku zote, nasi tutalishukuru jina lako milele. (Selah)
In God will we make our boast all the day, and to your name will we give thanks for ever. (Pause)
9 Lakini sasa umetutupa na kutufedhehesha, na hauendi na majeshi yetu.
But now you have cast off, and put us to shame; and you will not go forth with our hosts.
10 Umetufanya kuwakimbia maadui zetu; na wale watuchukiao huchukua vitu vyetu vya thamani kwa ajili yao wenyewe.
You have turned us back before our enemies; and they that hated us spoiled for themselves.
11 Umetufanya kama kondoo aliyeandaliwa kwa ajili ya chakula na umetutawanya kati ya mataifa.
You made us as sheep for meat; and you scattered us amongst the nations.
12 Wewe unawauza watu wako bure; kwa kufanya hivyo haukupata faida.
You have sold your people without price, and there was no profit by their exchange.
13 Wewe umetufanya kukemewa na majirani zetu, kuchekwa, na kudhihakiwa na wale wanao tuzunguka.
You have made us a reproach to our neighbours, a scorn and derision them that are round about us.
14 Umetufaya kituko kati ya mataifa, .......................................................
You have made us a proverb amongst the Gentiles, a shaking of the head amongst the nations.
15 Siku zote fedheha yangu iko mbele yangu, na aibu ya uso wangu imenifunika
All the day my shame is before me, and the confusion of my face has covered me,
16 kwa sababu ya sauti yake iliyo kemea na kutukana, kwa sababu ya adui na kisasi.
because of the voice of the slanderer and reviler; because of the enemy and avenger.
17 Yote haya yametupata sisi; bado hatukukusahau wewe wala kulikosea agano lako.
All these things are come upon us: but we have not forgotten you, neither have we dealt unrighteously in your covenant.
18 Mioyo yetu haikukengeuka; hatua zetu hazikuiacha njia yako.
And our heart has not gone back; but you have turned aside our paths from your way.
19 Bali wewe umetuadhibu vikali katika mahali pa mbweha na kutufunika na uvuli wa mauti.
For you have laid us low in a place of affliction, and the shadow of death has covered us.
20 Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetu au kueneza mikono yetu kwa Mungu mgeni,
If we have forgotten the name of our God, and if we have spread out our hands to a strange god; shall not God search these things out?
21 Mungu asingeligundua hili? Kwa maana yeye anazijua siri za moyo.
for he knows the secrets of the heart.
22 Hakika, kwa ajili ya jina lako tutauawa siku zote; tunahesabiwa kuwa kondoo kwa ajili ya kuchinjwa.
For, for your sake we are killed all the day long; we are counted as sheep for slaughter.
23 Bwana, amka, kwa nini unalala? Inuka, usitutupe moja kwa moja.
Awake, therefore sleep you, O Lord? arise, and do not cast [us] off for ever.
24 Kwa nini unaficha uso wako na kusahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu?
Therefore turn you your face away, [and] forget our poverty and our affliction?
25 Kwa maana tumeyeyushwa kwenye mavumbi; miili yetu imeshikamana na ardhi.
For our soul has been brought down to the dust; our belly has cleaved to the earth.
26 Inuka utusaidie na utuokoe kwa ajili ya uaminifu wa agano lako.
Arise, O Lord, help us, and redeem us for your name's sake.

< Zaburi 44 >