< Zaburi 4 >

1 Unijibu nikuitapo, Mungu wa haki yangu; uniokoe niwapo katika hatari. Unihurumie na usikie maombi yangu.
To the chief Musician on Neginoth, A Psalm of David. Hear me when I call, O God of my righteousness: thou hast enlarged me when I was in distress; have mercy upon me, and hear my prayer.
2 Ninyi watu, mpaka lini mtaiabisha heshima yangu? Mpaka lini mtaendelea kupenda kile kisicho stahili na kutafuta uongo?
O ye sons of men, how long will ye turn my glory into shame? how long will ye love vanity, and seek after falsehood? (Selah)
3 Lakini mjue ya kuwa Yahweh huchagua watu wa kimungu kwa ajili yake. Nitakapo mwita Yahwe atasikia.
But know that the LORD hath set apart him that is godly for himself: the LORD will hear when I call to him.
4 Tetemekeni na kuogopa, lakini msitende dhambi! Tafakarini mioyoni mwenu kwenye vitanda vyenu na muwe kimya.
Stand in awe, and sin not: commune with your own heart upon your bed, and be still. (Selah)
5 Toeni matoleo ya haki na muweke imani yenu katika Yahweh.
Offer the sacrifices of righteousness, and put your trust in the LORD.
6 Wengi husema, “Ni nani atakaye tuonyesha chochote kilicho kizuri?” Yahweh, utuangazie nuru ya uso wako.
There are many that say, Who will show us any good? LORD, lift thou upon us the light of thy countenance.
7 Umeupa moyo wangu furaha kuu kuliko wao wanapozidishiwa nafaka na divai mpaya.
Thou hast put gladness in my heart, more than in the time when their grain and their wine increased.
8 Ni amani kuwa nitajilaza na kusinzia, kwako pekee, Yahweh, nifanye kuwa salama kabisa.
I will both lie down in peace, and sleep: for thou only, LORD, makest me dwell in safety.

< Zaburi 4 >