< Zaburi 4 >

1 Unijibu nikuitapo, Mungu wa haki yangu; uniokoe niwapo katika hatari. Unihurumie na usikie maombi yangu.
To the chief Musician. On stringed instruments. A Psalm of David. When I call, answer me, O God of my righteousness: in pressure thou hast enlarged me; be gracious unto me, and hear my prayer.
2 Ninyi watu, mpaka lini mtaiabisha heshima yangu? Mpaka lini mtaendelea kupenda kile kisicho stahili na kutafuta uongo?
Ye sons of men, till when is my glory [to be put] to shame? [How long] will ye love vanity, will ye seek after a lie? (Selah)
3 Lakini mjue ya kuwa Yahweh huchagua watu wa kimungu kwa ajili yake. Nitakapo mwita Yahwe atasikia.
But know that Jehovah hath set apart the pious [man] for himself: Jehovah will hear when I call unto him.
4 Tetemekeni na kuogopa, lakini msitende dhambi! Tafakarini mioyoni mwenu kwenye vitanda vyenu na muwe kimya.
Be moved with anger, and sin not; meditate in your own hearts upon your bed, and be still. (Selah)
5 Toeni matoleo ya haki na muweke imani yenu katika Yahweh.
Offer sacrifices of righteousness, and confide in Jehovah.
6 Wengi husema, “Ni nani atakaye tuonyesha chochote kilicho kizuri?” Yahweh, utuangazie nuru ya uso wako.
Many say, Who shall cause us to see good? Lift up upon us the light of thy countenance, O Jehovah.
7 Umeupa moyo wangu furaha kuu kuliko wao wanapozidishiwa nafaka na divai mpaya.
Thou hast put joy in my heart, more than in the time that their corn and their new wine was in abundance.
8 Ni amani kuwa nitajilaza na kusinzia, kwako pekee, Yahweh, nifanye kuwa salama kabisa.
In peace will I both lay me down and sleep; for thou, Jehovah, alone makest me to dwell in safety.

< Zaburi 4 >