< Zaburi 4 >

1 Unijibu nikuitapo, Mungu wa haki yangu; uniokoe niwapo katika hatari. Unihurumie na usikie maombi yangu.
For the End, a Song of David amongst [the ]Psalms. When I called upon [him], the God of my righteousness heard me: you have made room for me in tribulation; pity me, and listen to my prayer.
2 Ninyi watu, mpaka lini mtaiabisha heshima yangu? Mpaka lini mtaendelea kupenda kile kisicho stahili na kutafuta uongo?
O you sons of men, how long [will you be] slow of heart? therefore do you love vanity, and seek falsehood? (Pause)
3 Lakini mjue ya kuwa Yahweh huchagua watu wa kimungu kwa ajili yake. Nitakapo mwita Yahwe atasikia.
But know you that the Lord has done wondrous things for his holy one: the Lord will hear me when I cry to him.
4 Tetemekeni na kuogopa, lakini msitende dhambi! Tafakarini mioyoni mwenu kwenye vitanda vyenu na muwe kimya.
Be you angry, and sin not; feel compunction upon your beds for what you say in your hearts. (Pause)
5 Toeni matoleo ya haki na muweke imani yenu katika Yahweh.
Offer the sacrifice of righteousness, and trust in the Lord.
6 Wengi husema, “Ni nani atakaye tuonyesha chochote kilicho kizuri?” Yahweh, utuangazie nuru ya uso wako.
Many say, Who will show us good things? the light of your countenance, O Lord, has been manifested towards us.
7 Umeupa moyo wangu furaha kuu kuliko wao wanapozidishiwa nafaka na divai mpaya.
You have put gladness into my heart: they have been satisfied with the fruit of their corn and wine and oil.
8 Ni amani kuwa nitajilaza na kusinzia, kwako pekee, Yahweh, nifanye kuwa salama kabisa.
I will both lie down in peace and sleep: for you, Lord, only have caused me to dwell securely.

< Zaburi 4 >