< Zaburi 36 >

1 Dhambi hunena kama unabii katika moyo wa mwovu; machoni mwake hamna hofu ya Mungu.
La transgresión del impío habla a su corazón. No hay temor a ʼElohim delante de sus ojos.
2 Kwa maana yeye hujifariji mwenyewe, akifikiria kuwa dhambi zake hazitagundulika na kuchukiwa.
Se jacta ante sus propios ojos De que su iniquidad no será descubierta ni aborrecida.
3 Maneno yake ni yenye dhambi na udanganyifu; hataki kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
Las palabras de su boca son iniquidad y engaño. Dejó de ser sabio, de hacer el bien.
4 Alalapo kitandani, hupanga namna ya kutenda dhambi; yeye hukaa nje kwenye nja ya uovu; yeye hakatai uovu.
Trama iniquidad sobre su cama. Se mantiene en camino no bueno. No aborrece lo malo.
5 Uaminifu wa agano lako, Yahwe, unafika mbinguni; uaminifu wako unafika mawinguni.
Oh Yavé, tu misericordia llega hasta el cielo, Y hasta las nubes tu fidelidad.
6 Haki yako ni kama milima ya Mungu; hukumu yako ni kama kina kirefu. Yahwe, wewe huwahifadhi wote wanadamu na wanyama.
Tu justicia es como las montañas de ʼEL, Tus juicios, como inmenso abismo. Tú, oh Yavé, preservas al hombre y la bestia.
7 Ni jinsi gani uaminifu wa aganao lako ni wa thamani, Mungu! Watu hukimbilia usalama chini ya uvuli wa mbawa zako.
¡Oh ʼElohim, cuán preciosa es tu misericordia! Por eso los hombres se amparan bajo la sombra de tus alas.
8 Nao watatoshelezwa tele na utajiri wa chakula nyumbani mwako; utawafanya wanywe kutoka katika mto wa baraka zako za thamani.
Son plenamente saciados con la abundancia de tu casa, Les das de beber del torrente de tus delicias.
9 Kwa kuwa mna chemichemi ya uzima; na katika mwanga wako tutaiona nuru.
Porque contigo está el manantial de la vida. En tu luz vemos la luz.
10 Uupanue uaminifu wa agano lako kikamilifu kwa wale wanao kujua wewe, ulinzi wako uwe juu ya wanyoofu wa moyo.
Extiende tu misericordia a los que te conocen, Y tu justicia a los rectos de corazón.
11 Usiuache mguu wa mwenye kiburi unisogelee. Usiiache mkono wa mwovu unitoweshe.
No me alcance el pie de la soberbia, Ni me mueva la mano del inicuo.
12 Kule wafanyao maovu wameanguka; wameharibiwa hawawezi kuinuka.
Ahí cayeron los que obran iniquidad, Fueron derribados, Y no pueden levantarse.

< Zaburi 36 >