< Zaburi 31 >

1 Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. In wewe, Yahwe, nakimbilia usalama; usiniache niaibishwe. Katika haki yako uniokoe.
For the end, a Psalm of David, [an utterance] of extreme fear. O Lord, I have hoped in you; let me never be ashamed: deliver me in your righteousness and rescue me.
2 Unisikie; uniokoe haraka; uwe mwamba wangu wa usalama, ngome ya kuniokoa.
Incline your ear to me; make haste to rescue me: be you to me for a protecting God, and for a house of refuge to save me.
3 Kwa kuwa wewe ni mwamba wangu na ngome yangu; kwa hiyo kwa ajili ya jina lako, uniongoze na unielekeze.
For you are my strength and my refuge; and you shall guide me for your name's sake, and maintain me.
4 Unitoe katika mtego ambao wameuficha kwa ajili yangu, kwa kuwa wewe ni usalama wangu.
You shall bring me out of the snare which they have hidden for me; for you, O Lord, are my defender.
5 Mikononi mwako naikabidhi roho yangu; nawe utaniokoa, Yahwe, mwenye kuaminika.
Into your hands I will commit my spirit: you have redeemed me, O Lord God of truth.
6 Ninawachukia wale wanaotumikia miungu isiyo na maana, bali ninaamini katika Yahwe.
You has hated them that idly persist in vanities: but I have hoped in the Lord.
7 Nitafurahi na kushangilia katika uaminifu wa agano lako, kwa kuwa uliyaona mateso yangu; wewe uliijua dhiki ya moyo wangu.
I will exult and be glad in your mercy: for you have looked upon mine affliction; you have saved my soul from distresses.
8 Wewe haujaniweka kwenye mkono wa maadui zangu. Nawe umeiweka miguu yangu mahali pa wazi papana.
And you have not shut me up into the hands of the enemy: you have set my feet in a wide place.
9 Uniurumie, Yahwe, kwa maana niko katika dhiki; macho yangu yanafifia kwa huzuni pamoja na moyo wangu na mwili wangu.
Pity me, O Lord, for I am afflicted: my eye is troubled with indignation, my soul and by belly.
10 Kwa kuwa maisha yangu yamechoshwa kwa huzuni na miaka yangu kwa kuugua kwangu. Nimekuwa dhaifu kwa sababu ya dhambi zangu, na mifupa yangu inachakaa.
For my life is spent with grief, and my years with groanings: my strength has been weakened through poverty, and my bones are troubled.
11 Kwa sababu ya maadui zangu wote, watu wananibeza; majirani zangu wanaishangaa hali yangu, na wale wanao nifahamu wanashtuka. Wale wanionao mitaani hunikimbia.
I became a reproach amongst all mine enemies, but exceedingly so to my neighbours, and a fear to mine acquaintance: they that saw me without fled from me.
12 Nimesahaulika kama mtu aliye kufa ambaye hakuna mtu anaye mfikiria. Niko kama chungu kilicho pasuka.
I have been forgotten as a dead man out of mind: I am become as a broken vessel.
13 Kwa maana nimesikia minong'ono ya wengi, habari za kutisha kutoka pande zote kwa pamoja wamepanga njama kinyume na mimi. Wao wanapanga njama ya kuniua.
For I heard the slander of many that lived round about: when they were gathered together against me, they took counsel to take my life.
14 Bali mimi ninakuamini wewe, Yahwe; Ninasema, “Wewe ni Mungu wangu.”
But I hoped in you, O Lord: I said, You are my God.
15 Hatima yangu iko mikononi mwako. Uniokoe mikononi mwa maadui zangu na wale wanao nifukuzia.
My lots are in your hands: deliver me from the hand of mine enemies,
16 Nuru ya uso wako imuangazie mtumishi wako; uniokoe katika uaminifu wa agano lako.
and from them that persecute me. Make your face to shine upon your servant: save me in your mercy.
17 Usiniache niaibishwe, Yahwe; kwa maana ninakuita wewe! Waovu waaibishwe! Na wanyamaze kimya kuzimuni. (Sheol h7585)
O Lord, let me not be ashamed, for I have called upon you: let the ungodly be ashamed, and brought down to Hades. (Sheol h7585)
18 Na inyamazishwe midomo midanganyifu ambayo husema maneno mabaya kuhusu watu wenye haki huku wakiwa na kiburi na dharau.
Let the deceitful lips become dumb, which speak iniquity against the righteous with pride and scorn.
19 Uzuri wako ni wa namna gani nao umeuhifadhii kwa ajili ya wale wanao kuheshimu sana, ambao wewe huufanya kwa ajili ya wale ambao hukimbilia kwako kwa ajili ya usalama mbele ya watoto wote wa wanadamu!
How abundant is the multitude of your goodness, O Lord, which you have laid up for them that fear you! you have wrought [it] out for them that hope on you, in the presence of the sons of men.
20 Katika makao ya uwepo wako, wewe huwaficha mbali na njama za watu. Wewe huwaficha mahali salama na ndimi zenye vurugu.
You will hide them in the secret of your presence from the vexation of man: you will screen them in a tabernacle from the contradiction of tongues.
21 Atukuzwe Yahwe, kwa maana yeye alinionesha maajabu ya uaminifu wa agano lake mahali nilipoishi.
Blessed be the Lord: for he has magnified his mercy in a fortified city.
22 Ingawa kwa haraka zangu nilisema, “Nimeondolewa machoni pako,” bali wewe ulisikia kusihi kwangu nilipokulilia wewe.
But I said in my extreme fear, I am cast out from the sight of your eyes: therefore you did listen, O Lord, to the voice of my supplication when I cried to you.
23 Enyi wafuasi waaminifu, mpendeni Yahwe, Yahwe huwalinda waaminifu, lakini huwalipa wakaidi ipasavyo.
Love the Lord, all you his saints: for the Lord seeks for truth, and renders [a reward] to them that deal very proudly.
24 Iweni imara na jasiri, ninyi nyote mnao mwamini Mungu kuwasaidia.
Be of good courage, and let your heart be strengthened, all you that hope in the Lord.

< Zaburi 31 >