< Zaburi 29 >

1 Mpeni sifa Yahwe, enyi wana wa Mungu! Mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
Ascribe to Adonai, you sons of the mighty, ascribe to Adonai kavod ·weighty glory· and strength.
2 Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili. Mpigieni magoti Yahwe katika mapambo ya utakatifu.
Ascribe to Adonai the kavod ·weighty glory· due to his name. Hawa ·Bow low, prostrate· to worship Adonai in holy array.
3 Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
Adonai’s voice is on the waters. The God of kavod ·weighty glory· thunders, even Adonai on many waters.
4 Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
Adonai’s voice is powerful. Adonai’s voice is full of majesty.
5 Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
Adonai’s voice breaks the cedars. Yes, Adonai breaks in pieces the cedars of Lebanon.
6 Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
He makes them also to skip like a calf; Lebanon and Sirion like a young, wild ox.
7 Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
Adonai’s voice strikes with flashes of lightning.
8 Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
Adonai’s voice shakes the wilderness. Adonai shakes the wilderness of Kadesh.
9 Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
Adonai’s voice makes the deer calve, and strips the forests bare. In his temple everything says, “Kavod ·Weighty glory·!”
10 Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
Adonai sat enthroned at the Flood. Yes, Adonai sits as King forever.
11 Yahwe huwatia nguvu watu wake; Yahwe huwa bariki watu wake na amani.
Adonai will give strength to his people. Adonai will bless his people with peace.

< Zaburi 29 >