< Zaburi 26 >

1 Unihukumu mimi, Yahwe, kwa kuwa nimeenenda katika uadilifu; nimeamini katika Yahwe bila kusita.
Of David - vindicate me O Yahweh for I in integrity my I have walked and in Yahweh I have trusted not I will slip.
2 Unichunguze, Yahwe, na unijaribu; uujaribu usafi wa sehemu zangu za ndani na moyoni mwangu!
Test me O Yahweh and put to [the] test me (test! *Qk) kidneys my and heart my.
3 Kwa maana uaminifu wa agano lako uko mbele ya macho yangu, na mwenendo wangu ni katika uaminifu wako.
For covenant loyalty your [is] to before eyes my and I walk about in faithfulness your.
4 Mimi sichangamani na watu waovu, wala sichangamani na watu wanafiki.
Not I sit with men of falsehood and with [those who] conceal themselves not I go.
5 Ninachukia waovu, na siishi na waovu.
I hate [the] assembly of evil-doers and with wicked [people] not I sit.
6 Ninaosha mikono yangu kounesha sina hatia, na kuikaribia madhabahu yako, Yahwe,
I wash in innocence hands my and I go around altar your O Yahweh.
7 kuimba wimbo wa sauti ya sifa na kutoa taarifa ya matendo yako yote ya ajabu.
To make heard a sound of thanksgiving and to recount all wonders your.
8 Yahwe, ninaipenda nyumba ninayoishi, mahali ambapo utukufu wako unaishi!
O Yahweh I love [the] habitation of house your and [the] place of [the] dwelling of glory your.
9 Usiniangamize pamoja na wenye dhambi, au maisha yangu na watu wenye kiu ya kumwaga damu,
May not you remove with sinners life my and with people of blood life my.
10 ambao katika mikono yao kuna njama, na ambao mkono wa kuume umejaa rushwa.
[those] whom [is] in Hands their wickedness and right [hand] their it is full a bribe.
11 Lakini kwangu mimi, nitaenenda katika uadilifu; uniokoe na unihurumie.
And I in integrity my I will walk redeem me and show favor to me.
12 Miguu yangu husimama sehemu salama; katika kusanyiko la watu nitambariki Yahwe!
Foot my it has stood on level ground in assemblies I will bless Yahweh.

< Zaburi 26 >