< Zaburi 25 >

1 Kwako, Yahwe, nayainua maisha yangu!
Pesem Davidova: K tebi, Gospod, dvigam dušo svojo.
2 Mungu wangu, ninaamini katika wewe. Usiniache niaibishwe; usiwaache maadui zangu wafurahie ushindi wao kwangu.
Bog moj, v té zaupam, naj se ne osramotim, sovražniki moji naj se ne radujejo nad mano.
3 Asiaibishwe mtu yeyote anaye kutumaini bali waaibishwe wale watendao hila bila sababu!
Tudi kdor čaka tebe, naj se ne osramoti; osramoté se naj, kateri izdajalsko ravnajo po krivem.
4 Unijulishe njia zako, Yahwe; unifundishe njia zako.
Pota svoja mi kaži, Gospod; steze svoje úči me.
5 Uniongoze kwenye kweli yako na unifundishe, kwa kuwa wewe ni Mungu wa wokovu wangu; ninakutumainia wewe siku zote za maisha yangu.
Daj, da hodim po resnici tvoji, in úči me; ker ti si Bog blaginje moje, tebe čakam ves dan.
6 Kumbuka, Yahwe, matendo yako ya huruma na uaminifu wa agano lako; kwa kuwa vimekuwapo siku zote.
Spomni se usmiljenja svojega, Gospod, in milosti svojih, da so od vekomaj.
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala uasi wangu; Uniweke akilini mwako pamoja na uaminifu wa agano kwa zababu ya uzuri wa wako, Yahwe!
Grehov mladosti moje in pregreškov mojih ne spominjaj se; po milosti svoji spominjaj se me ti, zavoljo dobrote svoje, Gospod.
8 Yahwe ni mzuri na mwenye haki; kwa hiyo yeye huwafundisha njia mwenye dhambi.
Dober in pravičen je Gospod: zatorej uči grešnike pot;
9 Yeye huwaelekeza wanyenyekevu kwa kile kilicho sahihi na yeye huwafundisha wao njia yake.
Dela, da hodijo krotki po pravici, in krotke uči pot svojo.
10 Njia zote za Yahwe ni za upendo wa kudumu na niaminifu kwa wote wanao tunza agano na maagizo ya amri zake.
Vse steze Gospodove so milost in zvestoba njim, ki hranijo zavezo njegovo in pričanja njegova.
11 Kwa ajili ya jina lako, Yahwe, unisamehe dhambi zangu, kwa kuwa ni nyingi mno.
Zavoljo imena svojega, Gospod, bodeš torej prizanesel krivici moji, ker velika je.
12 Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
Kakošen bode mož tisti, kateri se boji Gospoda, ki ga uči, katero pot naj izvoli?
13 Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
Duša njegova bode prenočevala v dobrem, in seme njegovo bode dedovalo deželo.
14 Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
Skrivnost Gospodova biva pri njih, ki se ga bojé, in zaveza njegova, da po izkušnji priča zanje.
15 Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
Oči moje gledajo neprestano v Gospoda; ker on potegne iz mreže noge moje.
16 Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
Ozri se v mé, in milost mi stóri; ker samoten sem in ubožen.
17 Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!
Stiske srca mojega se razširjajo; iz nadlog mojih potegni me.
18 Tazama mateso yangu na taabu yangu; unisamehe dhambi zangu zote.
Poglej siromaštvo moje in težavo mojo; in odpusti vse grehe moje.
19 Ona maadui zangu, kwa maana ni wengi; wananichukia kwa chuki ya kikatili.
Ozri se v sovražnike moje, ker močneji so; in s hudim sovraštvom me sovražijo.
20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe; usiniache niaibishwe, Kwa kuwa kwako nakimbilia usalama!
Reši dušo mojo in otmi me; naj se ne osramotim, ker pribegam k tebi.
21 Uadilifu na unyofu vinihifadhi, kwa kuwa nina kutumainia wewe.
Poštenost naj me brani in pravica, ker tebe čakam.
22 Mungu, uiokoe Israeli, na shida yake yote!
Reši, Bog, Izraela vseh zatiranj njegovih.

< Zaburi 25 >