< Zaburi 25 >

1 Kwako, Yahwe, nayainua maisha yangu!
In finem, Psalmus David. Ad te Domine levavi animam meam:
2 Mungu wangu, ninaamini katika wewe. Usiniache niaibishwe; usiwaache maadui zangu wafurahie ushindi wao kwangu.
Deus meus in te confido, non erubescam:
3 Asiaibishwe mtu yeyote anaye kutumaini bali waaibishwe wale watendao hila bila sababu!
Neque irrideant me inimici mei: etenim universi, qui sustinent te, non confundentur.
4 Unijulishe njia zako, Yahwe; unifundishe njia zako.
Confundantur omnes iniqua agentes supervacue. Vias tuas Domine demonstra mihi: et semitas tuas edoce me.
5 Uniongoze kwenye kweli yako na unifundishe, kwa kuwa wewe ni Mungu wa wokovu wangu; ninakutumainia wewe siku zote za maisha yangu.
Dirige me in veritate tua, et doce me: quia tu es Deus salvator meus, et te sustinui tota die.
6 Kumbuka, Yahwe, matendo yako ya huruma na uaminifu wa agano lako; kwa kuwa vimekuwapo siku zote.
Reminiscere miserationum tuarum Domine, et misericordiarum tuarum, quæ a sæculo sunt.
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala uasi wangu; Uniweke akilini mwako pamoja na uaminifu wa agano kwa zababu ya uzuri wa wako, Yahwe!
Delicta iuventutis meæ, et ignorantias meas ne memineris. Secundum misericordiam tuam memento mei tu: propter bonitatem tuam Domine.
8 Yahwe ni mzuri na mwenye haki; kwa hiyo yeye huwafundisha njia mwenye dhambi.
Dulcis et rectus Dominus: propter hoc legem dabit delinquentibus in via.
9 Yeye huwaelekeza wanyenyekevu kwa kile kilicho sahihi na yeye huwafundisha wao njia yake.
Diriget mansuetos in iudicio: docebit mites vias suas.
10 Njia zote za Yahwe ni za upendo wa kudumu na niaminifu kwa wote wanao tunza agano na maagizo ya amri zake.
Universæ viæ Domini, misericordia et veritas, requirentibus testamentum eius et testimonia eius.
11 Kwa ajili ya jina lako, Yahwe, unisamehe dhambi zangu, kwa kuwa ni nyingi mno.
Propter nomen tuum Domine propitiaberis peccato meo: multum est enim.
12 Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
Quis est homo qui timet Dominum? legem statuit ei in via, quam elegit.
13 Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
Anima eius in bonis demorabitur: et semen eius hereditabit terram.
14 Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
Firmamentum est Dominus timentibus eum: et testamentum ipsius ut manifestetur illis.
15 Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
Oculi mei semper ad Dominum: quoniam ipse evellet de laqueo pedes meos.
16 Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
Respice in me, et miserere mei: quia unicus et pauper sum ego.
17 Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!
Tribulationes cordis mei multiplicatæ sunt: de necessitatibus meis erue me.
18 Tazama mateso yangu na taabu yangu; unisamehe dhambi zangu zote.
Vide humilitatem meam, et laborem meum: et dimitte universa delicta mea.
19 Ona maadui zangu, kwa maana ni wengi; wananichukia kwa chuki ya kikatili.
Respice inimicos meos quoniam multiplicati sunt, et odio iniquo oderunt me.
20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe; usiniache niaibishwe, Kwa kuwa kwako nakimbilia usalama!
Custodi animam meam, et erue me: non erubescam, quoniam speravi in te.
21 Uadilifu na unyofu vinihifadhi, kwa kuwa nina kutumainia wewe.
Innocentes et recti adhæserunt mihi: quia sustinui te.
22 Mungu, uiokoe Israeli, na shida yake yote!
Libera Deus Israel ex omnibus tribulationibus suis.

< Zaburi 25 >