< Zaburi 24 >

1 Nchi ni ya Yahwe, na vyote viijazavyo, dunia, na wote wakaao ndani yake.
Die Erde ist Jehovahs, und ihre Fülle, die Welt, und die darauf wohnen.
2 Kwa kuwa yeye aliianzisha juu ya bahari na kuiimarisha juu ya mito.
Denn Er hat auf die Meere sie gegründet, und auf den Flüssen sie festgestellt.
3 Ni nani atakaye panda mlima wa Yahwe? Ni nani atakaye simama patakatifu pake?
Wer wird hinaufgehen auf den Berg Jehovahs, und wer wird aufstehen am Orte Seiner Heiligkeit?
4 Yeye ambaye ana mikono misafi na moyo safi; ambaye hajauinua uongo, na haja apa kiapo ili kudanganya.
Wer unschuldige Hände hat und lauteren Herzens ist, der seine Seele nicht erhebt auf Eitles und nicht schwört zum Trug.
5 Yeye atapokea baraka kutoka kwa Yahwe na haki kutoka kwa Mungu wa wokovu wake.
Der wird empfangen Segen von Jehovah, und Gerechtigkeit vom Gotte seines Heils.
6 Kizazi cha wale wamtafutao Mungu ni kama hiki, wale ambao wanautafuta uso wa Mungu wa Yakobo.
Dies das Geschlecht, das Ihm nachfragt, das Dein Angesicht sucht, o Jakob. (Selah)
7 Inueni vichwa vyenu, ninyi malango; muinuliwe juu, milango ya milango ya kudumu, ili kwamba Mfalme wa utukufu aweze kuingia!
Erhebt eure Häupter, ihr Tore, und erhebt euch, ihr ewigen Pforten, daß einziehe der König der Herrlichkeit.
8 Huyu Mfalme wa utukufu ni nani? Yahwe, mwenye nguvu na uweza; Yahwe, mwenye uweza katika vita.
Wer ist dieser König der Herrlichkeit? Jehovah, der Starke, der Held, Jehovah, der Held im Streite.
9 Inueni vichwa vyenu, ninyi malango; muinuliwe juu, milango ya kudumu, ili kwamba Mfalme wa utukufu aweze kuingia!
Erhebt eure Häupter ihr Tore, und erhebt euch, ihr ewigen Pforten, daß einziehe der König der Herrlichkeit.
10 Huyu Mfalme wa utukufu ni nani? Yahwe wa majeshi, yeye ni Mfalme wa utukufu.
Wer ist Er, dieser König der Herrlichkeit? Jehovah der Heerscharen ist es. Er ist der König der Herrlichkeit. (Selah)

< Zaburi 24 >